Spika wa Bunge Mhe. Samuel Sitta, anondoka Nchini LEO tarehe 9 Mei, 2010 kwenda nchini Uturiki kwa ziara ya mwaliko wa Spika wa Bunge la nchi hiyo, Mhe. Mehmet Ali Sahim. Katika Ziara hii, Mhe. Spika ataambatana na wabunge saba wanaounda chama cha ushirikiano baina ya Bunge la Uturuki na Bunge letu ambao ni:
1. Mhe. Wilson Masilingi (Mb)
2. Mhe. Lazaro Nyarandu (Mb)
3. Mhe. John Komba (Mb)
4. Mhe. Zuberi Maulid (Mb)
5. Mhe. Suzan Lyimo (Mb)
6. Mhe. Felista Bura (Mb)
7. Mhe. James Musalika (Mb)
Ziara hii ya Mhe. Spika Nchini Uturuki, inafuatia mwaliko wa Spika wa Nchi hiyo aliyoitoa Mwishoni mwa Mwezi March, 2010 na kuwasilishwa na Balozi wa Uturuki nchini Dkt. Sander Qubuz kwa Spika wa Bunge ikiwa ni jitihada za nchi hiyo kutoa fursa ya kipekee kwa viongozi wa kitanzania kutembelea nchi hiyo ili kuweka hamasa ya kukuza ushirikiano wetu kati ya Uturuki na Tanzania.
Katika ziara hii Ujumbe wa Tanzania ukiongozwa na Mhe. Spika utajionea shughuli mbalimbali za maendeleo na kiuchumi ikiwa ni jitihada za kuwahamasisha waturuki kuja kuwekeza chini katika sekta mbalimbali za maendeleo hususani katika sekta za viwanda vya nguo na utalii . Mwaliko huu wa ziara ya Mhe. Spika nchini uturuki utakuwa ni wapili kufanywa na viongozi wa Tanzania katika nchi hiyo ambapo awali Mapema Mwaka huu, Mhe. Rais wa Tanzania Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete alitembelea nchiyo kwa Mwaliko wa Rais wa Nchi hiyo. Ujumbe huu wa Tanzania unategemea kurejea nchini mwishoni mwa wiki hii.
Imetolewa na
Owen Mwandumbya
Afisa Habari wa Bunge
Owen Mwandumbya
Afisa Habari wa Bunge


Jamani naomba kuuliza, mheshimiwa John Komba atalipa nauli ya watu wangapi? Manake ni dhahiri kwamba seat moja haiwezi kumtosha na itabidi atumie viti viwili katika ndege.
ReplyDelete"MUHESHIMIWA" kwanini mnapenda kuabudiwa??ili neno halifai kabisa tumieni ndugu tu..aggggggrrrr
ReplyDeletemataifa mengine makubwa uko wala hawajiiti ili jina.iyo list vyama vingine wapo?
ovyo