Mama wa Waziri mkuu Alberina Kasanga akimzawadia kuku JK alipowatemebelea nyumbani kwao eneo la Kibaoni,wilayani Mpanda,mkoa wa rukwa jana mchana. Kulia ni Mzee Xaveri Kayanza Pinda,Baba ya Waziri mkuu mizengo Pinda
akiwa pamoja na wazazi wa Waziri Mkuu mhehimiwa mizengo Pinda huko nyumabni kwao Kibaoni, wilayani Mpanda,mkoa wa Rukwa jana mchana.Kushoto ni Mzee Xaveri Kayanza Pinda(80) Baba wa Waziri Mkuu na kulia ni Mama Albertina Kasanga(70) Mama wa Waziri Mkuu
Mtaalamu wa Maabara katika hospitali ya mkoa wa Rukwa bwana Dodea Mlenda akimpa maelezo Rais Jakaya Mrisho Kikwete jinsi mashine mpya za kisasa za uchunguzi wa maradhi zinavyofanya kazi muda mfupi baada ya Rais Kuzindua maabara ya kisasa katika hospitali ya mkoa wa Rukwa jana asubuhi.Maabara hiyo ya hospitali ya mkoa wa Rukwa ni kati ya maabara 23 zinazojengwa katika mikoa mbalimbali nchini kwa msaada wa shirika la Abbott Fund lenye makao yake nchini Marekani.Kushoto ni Mbunge wa Kwela Chrisant Mzindakaya na watatu kutoka kushoto ni Mwakilishi wa Waziri wa Afya Dr.Pamela Sawa.
JK akikata utepe kuzindua ujenzi wa mitambo mipya ya kuzalisha umeme mjini Sumbawanga jana asubuhi.Mitambo hiyo itauwezesha mji wa Sumbawanga na wilaya za jirani kupata umeme wa uhakika.Watatu kushoto ni Waziri wa Nishati na Madini William Ngeleja,wa kwanza kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO mhandisi Willoima Mhando na wane kushoto ni meneja mahusiano wa TANESCO Badra Masoud.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 12 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 20, 2010

    huyu waziri mkuu sio mwizi kabisa si unaona kwa wazazi wake kulivyo hongera pinda

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 20, 2010

    Mtoto wa mkulima kweli ana makuu...ingekuwa ni fisadi ungekuta wazazi wake wanaishi kwenye nyumba ya gorofa.Huyu na Sokoine tu ndiyo walikuwa wameka utaifa mbele.

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 20, 2010

    Je Je Je hawa ni wazazi wa Pinda kwa maana ya Kumzaa? Maana Pinda mwenyewe alizaliwa Mizengo Kayanza Peter Pinda (born August 12, 1948) hivyo kwa sasa ana miaka 62. Je kama mama yake ana miaka 70 basi alizaa akiwa na miaka 8? n baba yake ana miaka 80 je alizaa akiwa na miaka 18? Naomba majibu ili nijue hawa ni wazazi wa kumzaa waziri mkuu wetu au wazazi wadogo? Naomba ufahamu.

    ReplyDelete
  4. Wala usipate tabu ndugu yangu hapo juu hawa ni wazazi wake kabisa wa kumzaa nawajua tulikuwa majirani henzi hizo hapohapo Kibaoni Mpanda bigup wazee kwa kumlea kamanda Mizengo Peter Pinda kweli alitakiwa kuingia madarakani tangu zamani

    ReplyDelete
  5. AnonymousJune 20, 2010

    good question??? wadu tunaomba jibu ili tuendelee kuosha kinywaaaaaa??!!1

    ReplyDelete
  6. AnonymousJune 20, 2010

    cha ajabu kipi kama ni baba yake wanaume wazaa hata wakiwa na umri mdogo labda huyo ni mama yake mdogo yaani baba yake alioa mke mwingine

    ReplyDelete
  7. AnonymousJune 20, 2010

    Jamani Waziri Mkuu amefanana na mama yake. Hongera wazazi.

    ReplyDelete
  8. AnonymousJune 21, 2010

    Mimi Baba yangu ana miaka 58 mama yangu ana miaka 56 Mimi nina miaka 43 naomba mnijadili mimi na wazazi wangu...nakaa manzese kwa tumbo sina wadhifa wowote serikalini wala kwenye mashirika yenu ya umma, ninauza karanga mtaani!!!!

    ReplyDelete
  9. AnonymousJune 21, 2010

    Hii imenifurahisha sanaaaa. Si muda mrefu uliopita nilimuona Mheshimiwa Pinda akimjulia hali Mzee Edward Nsalamba, aliye kuwa mbunge wakati huo halafu tena namuona HE JK anawajulia hali wazazi wa Pinda. Hii inaonyesha wazi watu hawa walivyolelewa katika maadili mema ya upenda.Mi nilisoma na Vijana wa Mzee Nsalamba anayeitwa Christopher E. Nsalamba, na tuliishi majirani sana Mpanda kama ni mpenzi wa blog ya jamii basi anipe email tuwasiliane.

    ReplyDelete
  10. Mimi nadhani umri wa wazee wetu hawa umekosewa.Tujaalie mtu kuzaa akiwa na miaka 14 basi mama yetu huyo anatakiwa awe na miaka 76 na siyo 70 na baba awe kazaa akiwa na miaka 18 hapo kitaeleweka. vinginevyo mtuambie hawa ni awlezi wa Mizengo Kayanza na sio wazazi wa Mtoto wa mkulima mwenye umri wa miaka 62

    ReplyDelete
  11. AnonymousJune 21, 2010

    Wewe Mon Jun 21, 12:30:00 PM ujaweka email yako halafu unasema nikupe email tuwasiliane. Wewe vipi?

    ReplyDelete
  12. AnonymousJune 21, 2010

    haya je na haya majina ni ya kikwetu kwetu au ya kisumbiji sumbiji na portugal jamamani naona kuna XAVI NDANI HUMO?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...