Mr II (kulia) akila tano na mmoja wa waasisi wa Bongo Fleva MC Ryhmson kwenye kongamano
la muziki huko Bagamoyo siku za nyuma


MSANII wa Kizazi Kipya, Joseph Mbilinyi, al maarufu kama Mr II leo alikamatwa kama Breking Nyuuuzzzzz yetu ilivyoeleza awali, na kushikiliwa kwa zaidi ya masaa matano na Jeshi la Polisi kabla ya kuachiwa kwa dhamana kwa kile kilichoelezwa kuwa ni kutishia kuua kwa kutumia muziki wake.

Mr II alikumbwa na mkasa huo majira ya saa tano asubuhi kwenye viunga vya Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA), wakati akijiandaa kuwasilisha mada ya Muziki wa bongo fleva ulipotoka na hatma yake kwenye jukwaa la Sanaa linalofanyika kila Jumatatu kwenye ukumbi wa Baraza hilo.

Globu ya Jamii ambayo imeshuhudia Mr II akiwa chini ya ulinzi Makao Makuu ya Jeshi 'Wizara ya Mambo ya Ndani' kwa mahojiano. Hata hivyo jeshi hilo halikuwa tayari kutoa taarifa zozote kwa madai kuwa upelelezi bado unaendelea na utakapokamilika utaweka wazi suala hilo.

Hata hivyo habari kutoka kwa watu wa karibu na Mr II zinasema kuwa mwanamuziki huyo aliitwa kwa mahojiano tangu Alhamisi iliyopita na watu walinzi hao wa usalama wa raia lakini hakuitikia wito.

Inadaiwa Mr II amesambaza CD yenye nyimbo 14 aliyoipa jina la "Anti Virus Mix Tape" ambayo amekikashifu kituo kimoja cha redio ikiwa ni pamoja watangazaji na wakurugenzi wa kituo hicho.

Katika CD hiyo Mr II ameshirikiana na wasanii zaidi ya 10 akiwemo kama G – Solo, Mapacha na Mkoloni.

Akizungumza na Blog ya Jamii mara baada ya kuachiwa kwa dhamana majira ya saa 11 jioni Mr II alisema: “Nashukuru nimeachiwa kwa dhamana.

"Nimejidhamini mwenyewe. Nchi hii ina uonevu sana. Eti wanasema wamenikamata kwa tuhuma za kutishia kuua kwa maneno kwa kutumia mziki wangu.

"Wameniambia niripoti tena Polisi siku ya Jumatano kwa mahojiano zaidi na kwamba upelelezi wao bado unaendelea.”alisema Mr II.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 36 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 28, 2010

    ITS SO SAD; KUONA SYSTEM MBOVU LAKINI
    BADO HAWATAKI KUKOSOLEWA:
    ETI WANA USALAMA !!
    GO BACK TO SCHOOL:
    KEEP GOUING MR II ;DONT STOP THE REVOLUTION:

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 28, 2010

    mr suguuu usijali umewaambia ukwelii hasa yule R kazidi kuumiza wasanii, kwa nini kila msanii alalamike kuhusu yeye? weka wakili mzuri wa kukutetea safi sana umewachana laivu bila huruma
    mdau canada

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 28, 2010

    HAYA YOTE SABABU YA KUJIUNGA CHADEMA KHA!!!!!!!!

    ReplyDelete
  4. AnonymousJune 28, 2010

    sugu kiboko kuna kipengele kwenye huo wimbo kiliniacha hoiiiii.... na nimeaminia manake kuna mtangazaji mmoja huko kwenye hicho kituo, mkewe amepanga siku ya talaka anataka aangushe bonge la party na matarumbeta ati mtoto si rizki ndoa bubu alimradi siku hazigandi yani tunaingojea kweliiiii hiyo divosi party!!

    ReplyDelete
  5. AnonymousJune 28, 2010

    Comment yangu ndio umeibania sio Michuzi Yote KWeli sababu ya Chadema na Bifu lao na wale Radio Ya C na yule jamaa R michuzi usibanie bwana najuwa mnaogopa mbele ya mwenyezimungu mtajibu nini? Kama mdau hapo ju alivyosema Shule muhimu, MZ

    ReplyDelete
  6. AnonymousJune 28, 2010

    Mbona mafisadi hawawakamati hao mapolisi? Ama kweli inatakiwa kuwafukuza kazi mapolisi wote na kuanza na damu mpya. Kamateni mafisadi basi, si mnawafahamu? Ujinga mtupu.

    ReplyDelete
  7. AnonymousJune 28, 2010

    Huyu sugu muongo kuliko watu wote kila mahali anasema kuwa yeye ndio muasisi wa bongo fleva wakati sio kweli muasisi.muasisi wa bongo fleva ni saleh jabir.

    ReplyDelete
  8. AnonymousJune 28, 2010

    Vijana wenzangu kuweni makini na matumizi ya teknohama iwe Txt Mgs, emails, Youtube, facebook,Blogs, Radio,CDs, websites n.k maana huku ulaya kama Uingereza mambo yanaweza kuanzia ktk facebook na kuishia kushikana mitaani.

    Juzi tumezika kijana mmoja mtanzania, kisa kilianzia ktk facebook na kuishia mshikemshike mtaani tukampoteza dogo wa Kitanzania.

    Mdau
    Jijini London.

    ReplyDelete
  9. AnonymousJune 28, 2010

    Jamani haya mambo ya kumchana mtu abt ngoma hayafai, huu ni unyanyapaaji ambao actually ni kosa la jinai.

    anon Mon June 28, 08:27:00
    You r right, technolojia noma, na facebook inasave automatically kila kitu bora hata msn na yahoo mpaka uamue wewe kusave. Kesho keshokutwa mtu unataka kugombea uraisi au hata unakuwa a public figure of any sort, watu wanamwaga hadharani ujinga uliokuwa unachat ktk facebook.

    ReplyDelete
  10. AnonymousJune 28, 2010

    mweee Mungu tusaidie huu uhuni wa sirikali!!

    ila iko siku mtajibu tu mbele ya haki,hakuna marefu yasiyo na ncha!!

    simjua kiivo uyu sugu bt mh nna mashaka kama kweli amesambaza ujumbe wa kuua!!

    ReplyDelete
  11. AnonymousJune 28, 2010

    Sugu achana na longolongo za Bongo, rudi huku USA tupige Box. Jamaa watakumaliza hao, shauri yako

    ReplyDelete
  12. AnonymousJune 28, 2010

    Sugu moto chini... kichaa nakuaminia. Wajingawajinga wakina R wape ukweli wao wamezidi.Nakumbuka sana maneno yako uliyoniambia ulivyokua UK, Kuhusu muziki wa bongo jamaa wanaona kama wanaumiliki wao pamoja na wanamuziki wote......wachane tu mwanangu watu ukweli hawaupendi.

    ReplyDelete
  13. AnonymousJune 28, 2010

    Ndio maana nimekuwa raia wa U.S. kutokana na upumbavu mwingi unaoendelea Tanzania. Nchi ina wasomi wengi, tena wengi wao wamesoma hapa U.S., lakini cha kushangaza bado hakuna mabadiliko ya maana kijamii. Utasikia mkuu wa mkoa anatoa amri kwa polisi kumkamata fulani. Toka lini political figure akawafundisha polisi kazi? Huo ni upumbavu na abuse of power. Hapa U.S., hata Obama hawezi kuamuru polisi wamkamate fulani, kwa sababu katiba inasema wazi kuwa mtu atakamatwa pale tu panapokuwa na sababu ya kutosha (probable cause, 4th Ammendment). Kwa mfano, kama kuna mtu mitaani anasemekana ni mwizi au muuaji, hapa U.S. hawezi kukamatwa mpaka akutwe anaiba(live), au kuwepo ushaidi wa kutosha ambao utathibitishwa kitaalamu mahakamani kuwa amehusika moja kwa moja na tukio husika, kwa mfano, alama za vidole, au DNA, au video clips. Lakini Tanzania ni kawaida kwenye mikutano kusikia mkuu wa wilaya anamwamuru OCD amkamate fulani on the spot. Tatizo viongozi Tanzania elimu ni duni, alafu kwa bahati mbaya nao polisi elimu yao finyu, na pia kuna power/office abuse. Nasema tena, I am a proud American citizen of Tanzanian origin. Passport ya Tanzania ilisha expire zamani na sina mpango wa kui renew kwa sababu ya upumbavu na rushwa zinazoendelea Tanzania. I love USA. God Bless America!

    ReplyDelete
  14. AnonymousJune 28, 2010

    Ndiyo Maana Ankal Kamau anaitukana Tanzania. Yaani Mtu unalazimishwa kupenda chama fulani. Ukikataa unakamatwa?

    ReplyDelete
  15. AnonymousJune 28, 2010

    Hivi ndivyo unavyopatikana ushindi wa kishindo ktk chaguzi zetu.

    Ananikumbusha kijana mwingine Muro.

    Africa inahuzunisha.

    ReplyDelete
  16. AnonymousJune 28, 2010

    Ndo mana hata mimi nipo hapa UK nimemaliza masters nabeba Box Muda usogee niombe British passport coz its shame to be Tanzanian.

    ReplyDelete
  17. AnonymousJune 28, 2010

    poa kama hamtairusha hii lakini ata un unaesoma sasa ujumbe umefika najua kabisa ni claus fm 88.4 ndo wamemchana mr 2 hakuna ubishi maana ndo wana kihere here sna mimi nimemaliza na ndo yangu hayooo. wamenikera ka nini...........

    ReplyDelete
  18. AnonymousJune 28, 2010

    we mdau wa hapo juu,watu kama nyinyi ndio mnaoturudisha nyuma,kuchukua araia sio solution,solution ni sisi wabongo tunaokaa nnje kwenda bongo na kuchange hizo tabia mbovu za watanzania,mr 2 endeleza mapammbano ila tatizo bongo kuna kama kasecrety society inayo control vitu bongo na hao watu wanataka kila mtu awanyenyekee,sikubali afadhali niwe maskini kuliko kujipendekeza kwa watu wachache wajingawajinga,

    ReplyDelete
  19. AnonymousJune 28, 2010

    Kusema ukweli wimbo una eleweka na kama ni kukamatwa eti sababu kaimba he want's to kill right now, mbon ahuo usemi unatumika pia kwa kiswahili kama neneno la kwaidia sikuhizi??? Utakuta jamaa wanaongea na mtu anasema "DAH JAMAA KAUWA KISHENZI" kwa hiyo hao watu wafanywe nini??? Mi naona ni zaidi ya huo wimbo bwana hebu waseme ukweli. Lakini Sugu kawaidia yake kuimba ukweli.

    ReplyDelete
  20. AnonymousJune 29, 2010

    Sugu mwenyewe mbona kaisha kabisa kimuziki. Hata huo wimbo wenyewe anaimba off-key? Hata 2Pac mwenyewe alikuwa anatukana na kutishia kuua lakini alikuwa anabaki kwenye key aki-rap. Hii habari ya kumkamata ni upuuzi unaompa umaarufu asio nao. Kama kuna mtu anaukumbuka wimbo wowote mmoja wa Sugu autaje hapa! Hakuna. Jamaa hamna kitu, anaona wivu tu vijana kama Marlaw wanajenga nyumba wana magari kwa ajili ya muziki. Profesa Jay, Lady Jay Dee, wote wanakula bata kwa muziki. Muziki ni talent sio siasa. Wewe kama umekwisha usikimbilie siasa na kutukana watu ili urudi kwenye media.

    rap ya kutishia kuua hata huko marekani imepitwa na wakati. Huwezi kusema watu wana ngoma kwenye muziki, halafu unasema nchi ina uonevu. Ujinga mtupu! Rudi shule ^^^ mkubwa wewe!

    ReplyDelete
  21. AnonymousJune 29, 2010

    Lugha za "Kill" na "maza fwaka" ni nje ya utamaduni zetu.

    Kutaja jina la kampuni ya mtu, jina la mtu na kutoa kashfa ni makosa.

    Kimsingi sioni busara hapo wala hakuna kuonewa. Hata mimi ningemshitaki no matter wananchi watampa umaarufu kiasi gani.

    Wabongo tuwe na busara kama waliokaa kimya. Na sio kumpatia umaarufu alioutafuta kwa kuwaita watangazaji ni ma-gay nk. Too bad

    ReplyDelete
  22. AnonymousJune 29, 2010

    kuwa mtanzania ni kupoteza muda ukisema ukweli wanata kukuua.hv rais na wengine hawaoni huu upuuzi au?

    ReplyDelete
  23. AnonymousJune 29, 2010

    Mtu anaweza Kusema Leo Nitauwaaaaaaaaaaaaa Demuuuuuuuuuuu hapo najuwa humu asilimia kubwa mtakuwa mumenielewa kabisa! Ile Radio inachuki Binafsi tu Wale washamba wa Life ndio watainyenyekea.

    Watu wanapoteza Muda mwingi na Radio Clouds TRD mnaiuwa.

    ReplyDelete
  24. AnonymousJune 29, 2010

    i wanna kill right now,i wanna kill right,radio imejaa mashoga,watangazaji wanaliwa kama mboga hahahaha huu mstari umeniua kweli sugu(these lines have killed me right now)

    ReplyDelete
  25. AnonymousJune 29, 2010

    A LOT OF CRAP IN BONGO THIS IS ANOTHER ONE.AS SOON THE GUY DECLARED HE'S CHADEMA THEN THEY START HUNTING FOR HIM,BS.BY THE WAY THE MDAU THAT HAS GRABED US CITEZENSHIP,CONGRATU,IM FOLLOWING THE LIBENEKE,BONGO IS FULL OF B.S

    ReplyDelete
  26. AnonymousJune 29, 2010

    heheheheh pole sana Chadema toka huko
    ila yote tisa mkuu sheria inakuruhusu kujidhamini mwenyewe? hehehehehe dhamana si bail/sort of sponsorship mtu anayekua answerable ukitoroka/potea sasa ukijidhamini mwenyewe ukapotea mwenyewe nani wa kulaumiwa
    nenda ccm kaka

    ReplyDelete
  27. AnonymousJune 29, 2010

    huo mwimbo upo youtube ama tunaomba link na sisi tusikilize basi !!

    ReplyDelete
  28. AnonymousJune 29, 2010

    CHAGUA SI-SI-EMU MAISHA BORA KWA KILA M-TZ!

    ReplyDelete
  29. AnonymousJune 29, 2010

    Kinachonisikitisha hapa ni kwa jinsi polisi walivyokua makini kwa swala hili ambalo tunasema "personal issues" kati ya Mr. II na hicho kituo cha Radio. Mie ningetegemea hawa polisi wetu watoe kipau mbele kwa mambo ya msingi zaidi yenye kusaidia nchi. Sasa hivi ujambazi umekithiri, je wadhani hao polisi hawajui huo mtandao? Kwa nini wasipeleke nguvu zao huko? Sasa hivi kuna rushwa kwa ajili ya uchaguzi, watu wameshaanza kuneemeka kwa kuvuta mikwanja, kwani polisi hawalioni hili? Kuna ufisidi, madawa ya kulevya na uovu mwingi ambao unaipeleka Tanzania yetu pabaya, kwa nini hawa polisi wasijikite huko zaidi? Huku binafsi nasema ni kukosa dira kwa vyombo vyetu vya usalama, havijui vinataka kwenda wapi, viende vipi, na hata havitajua kama vimefika vinapotaka kwenda, na wala hawatajua wafanyeje wakishajua wamefika wanapokwenda.

    Mr. II na yeye akumbuke maneno unapoyatumia vibaya nayo ni zaidi ya kuua, kwa hiyo iwe funzo kwa wasanii wengine kujua namna ya kutumia maneno sahihi wanapotaka kufikisha ujumbe wao. Ila Mr. II kumbuka umejiunga Chadema, na siasa ya Tanzania bado sio ya kidemokrasia, bado tunakua wanafiki hatutaki kuambiana ukweli, na tukisema ukweli tunaonekana wabaya. Ila haya yana mwisho wake....!

    ReplyDelete
  30. AnonymousJune 29, 2010

    BONGO NOMA POLICE HAWANA AIBU,

    ReplyDelete
  31. AnonymousJune 29, 2010

    Mhh. Nafikiri cheche zaweza leta moto mkubwa.
    Nafikiri tatizo sio kujiunga CHADEMA
    Hizi ni hasira za maumivu ya kuhisi kuonewa hata kama huonewi. Chanzo MALARIA NO MORE.
    mimi nimesikiliza vizuri huo wimbo kwenye YOU TUBE, Nafikri watanzania tusishabikie kila kitu.
    Naunga mkono polisi kumkamata Mr. 2 na kwenda kumhoji kwani ametaja majina ya watu halisi,Hivi leo mmoja wa waliotajwa akidhurika nani wa kwanza kukamatwa?
    Mauaji ya Rwanda yalianza kwa mitindo ya aina hii vikiwepo na vituo vya redio vya aina ya alivyotaja Mr 2, lakini si yatupasa kujifunza kutokana na makosa?
    Pia huo mziki una lugha chafu zisizostahili kuimbwa hadharani katika nchi za kiafrika, Watz mliopo ughaibuni tusijisahau tukafikiri kila alichoimba 2pac kinafaa Tz, huo utakuwa ni ulimbukeni wa kuiga hata mambo yasiyofaa, Napata shida labda ningejua Mr 2 ana degree ya kitu gani, maanake kila taaluma kuna ethics zake na karibia zote zina fanana isipokuwa tofauti inakuja huyu ni daktari, Engineer n.k kwa hiyo kunakuwepo na nyongeza kulingana na fani.
    Nafikiri walio karibu na Mr 2 wajaribu kumshauri, kama ana ugomvi na hao jamaa na anaona wamemkashifu aende mahakamani akawashatiki au atumie njia nyingine ambayo haitamgharimu, sio kila siku ahisi anaonewa.
    Ninavyoelewa Usanii maana yake ni kuweka tungo kwenye mafumbo ili msikilizaji atumie akili kuchanganua, mimi na wewe tupate majibu tofauti katika kutafakari huo utunzi huo.

    ReplyDelete
  32. AnonymousJune 29, 2010

    MR II WEWE NI MWANAUME KATIKA WANAUME. NAKUPONGEZA WEWE NA N.SUMARI KWA KUJITOKEZA NA KUJIUNGA NA UPINZANI BILA WOGA WOWOTE AU KUGANGA NJAA KAMA WANAMUZIKI WENGINE.

    KEEP IT UP TUPO NYUMA YAKO HATA KUKULIPIA WAKILI.

    DONT STOP MPAKA KIELEWEKE.

    ReplyDelete
  33. AnonymousJune 29, 2010

    Ebwana eeh, hi cd inaitwa Antivirus Mix Tape ni balaa! Haiuzwi madukani ila inatambaa kama virus ya ukweli! Nimepata free copy kwenye internet cafe moja katikati ya jiji - sio mchezo maana ipo bomba kishenzi! Wapo artists kibao wa bongo fleva kama akina Sugu, Mkoloni, G-Solo na wengine wengi tuu - wazungu wanasemaga game on! Katika pitapita zangu online kwenye YouTube nikaikuta hii hapa http://www.youtube.com/watch?v=hiMGe2HYq2o

    ReplyDelete
  34. AnonymousJune 29, 2010

    Ama kweli Sugu sasa ameonesha kufikia ukingoni. Siyo yule II Proud aliyekuwa anatamba kwa kuelimisha jamii katika nyimbo zake. Huu wimbo inaonesha kupungukiwa na busara na hata uvumilivu. Aidha Sugu ameingia kwenye siasa hasa opposition akidhani ni kinga ya kufanya maovu na upuuzi. Sidhani hata hao CHADEMA wako tayari kufikiwa na ugeni uliokosa mwelekeo. CHADEMA si chaka la wahuni au wale walioishiwa, CHADEMA ni chama mbadala. Wimbo wa Sugu umeonesha upungufu mkubwa katika kuelimisha na kuburudisha jamii. Aidha maudhui yaliyomo katika wimbo huo ni matokeo ya mvutano binafsi katika yake yeye na Ruge na hii hakupaswa kuwa mwepesi kiasi cha kuiteremsha hadhi yake mbele ya jamii.
    Ningependa kumkumbusha Sugu na Jeshi la Polisi kuwa yule kijana aliyeuwa wanafunzi pale Virginia Tech alirekodi nia yake. Yule physical fitness trainer aliyeuwa pale kwenye PA alirekodi nia yake. Kwahiyo basi hii ni valid alert na haipaswi kupuuzwa.

    ReplyDelete
  35. AnonymousJune 29, 2010

    YAANI NILIPOKUONA TU UNAPOKEA KADI YA CHADEMA, SIMPLY NIKAJISEMEA LAZIMA UANGUSHIWE JUMBA BOVU. KUMBE KAMA UTANI NIMEKISIA UKWELI, BONGO TAMBARARE KWELI X2.

    ReplyDelete
  36. AnonymousJune 29, 2010

    Nchi iliojaa wajinga,ndio mambo hayo.sugu kawekwa ndani kwa kutishia kuua kutumia mziki wake!!wabongo longolongo tu,kesho mkiambiwa kuandamana mikia mnakunja.wacheni uoga,TZ inaangamia na wabongo tunaiona hivihivi!!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...