kwa mbele
kwa nyuma

Ankal.
Heshima kwako mkuu naomba niwekee haka kausafiri kwenye blog yetu.
ina wiki moja toka iingie jijini Dar.
inauzwa kwa sababu mwenye nayo alikosea hakuchagua Automatic Transmission, naye hapendi kutumia manual,hivyo anataka kurudisha gharama zake aangalie altenative ya kupata auto.
Imeingia ikiwa na kilometer 820000Km.
Manual Transmission
Subaru Forester ya mwaka 2004,
Black color
Imesajiliwa Tayari
Bei 16million.
Mawasiliano +255 714 979797

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 16 mpaka sasa

  1. Mdau unayeuza gari sina mpango wa kukuharibia soko lako.

    Kwasababu mimi siyo mtaalamu wa mambo ya magari na kwenye maisha yangu sijawahi kumiliki gari, ila tu napenda nijue ni kwasababu gani watu hapa Ulaya hawapendi kusikia habari ya magari Automatic transmission?

    ReplyDelete
  2. Unaitwa uzushi!eti kakosea kuchagua,siuseme tu umenunua ulaya unataka kuuzia wabongo upate faida vile wana zipapatikia.

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 09, 2010

    Kizushi na wewe wivu tu wa maisha yatakushinda mwanaume kazana kama wenzako, kazi majungu tu.

    ReplyDelete
  4. AnonymousJuly 09, 2010

    wacheti hivyo viroho vya korosho,kama hujawahi kumiliki gari hayo ni matatizo yako,hiyo ulaya ya wapi hawapendi auto,na ndio zimejaa kuliko manual,hata malori sasa mengi ni auto,huwezi kununua kaa kimya,sio kusaga maana hajalazimisha mtu kununua.

    ReplyDelete
  5. AnonymousJuly 09, 2010

    LAZIMA ENGINE ITAANGUKA CHINI KWA MTU ATAKAEINUNUA. KILOMETA LAKI 8 NA ISHIRINI ELFU?? 820,000KM? AU KUNA MAKOSA YA KUCHAPISHA!

    ReplyDelete
  6. AnonymousJuly 09, 2010

    Habari yako, hii habari ya magari kuuzwa kwa bei ya Mill 16 umeipata wapi mbona mnapenda sana kubabua watu na bei zenu za ajabu ajabu?.
    Subaru kama hii inauzwa si zaidi ya Usd 2500 huko japani na tena kama ukitafuta vizuri unaweza kupata mapaka chini ya hapo labda kama ni special option sawa vinginevyo bei yako si ya Kitanzania, hebu tuambie mpaka Mill 16 umenunua kiasi gani, usafiri na ushuru kiasi gani hadi kufikia hizo NOTI?.
    Mdau

    ReplyDelete
  7. AnonymousJuly 09, 2010

    Gari limetumika balaa KM 820000 c mchezo, peleka vyuma chakavu ndugu

    ReplyDelete
  8. AnonymousJuly 09, 2010

    Mmh!! Ngoja mie nikae pembeni maana nilipoona eti BEI POA niliwahi saana kuikimbia kuangalia! Baada ya kuona bei poa yenyewe Loooh!!! Sijui ni Bei poa ukilinganisha na nini haswa!!!!!! Ok lakini Vidole havilingani!! So aloandika na wengine ni Bei Poa lkn kwa sisi wengine Means different..........

    ReplyDelete
  9. AnonymousJuly 09, 2010

    Ndugu muuzaji, hilo gari kwa hizo kilometa 820,000 ni chuma chakavu, si gari!

    ReplyDelete
  10. AnonymousJuly 09, 2010

    JAMANI WANAJAMII KUNA MAKOSA SIO KILOMITA LAKI NANE NI ELFU THEMANINI NA 82000KLM

    ReplyDelete
  11. AnonymousJuly 09, 2010

    KUNAMAKOSA YA KIUCHAPAJI SI KILOMETA LAKI NANE NI ELFU THEMANINI NA MBILI PEKEE 82000KM

    ReplyDelete
  12. AnonymousJuly 09, 2010

    MDAU WA Tarehe Fri Jul 09, 07:50:00 AM..NINGEPENDA KUKUJULISHA KWAMBA HAKUNA GARI YA MODEL HII UTAIPATA KWA BEI HIYO NINGEPENDA KUPATA DATA ZAIDI ILI KAMA VIPI WENGINE TUAGIZE KUTOKA KWENYE SOURCE YAKO. NISHAWAHI KUAGIZA GARI KAMA HII LAST YEAR NIKIPIGA HESABU ZA USHURU NA UPLIFT ZA JAMAA ZETU WA TRA PAMOJA NA USAJIRI NA KILA KITU JAMA INAPUNGUA SANA NI LAKI NNE HIVI MWENYE UWEZO AJIMWAGE TU

    ReplyDelete
  13. AnonymousJuly 09, 2010

    Bwana Malkiyory ni kwamba, ulaya kwa sababu wana miundombinu mizuri huwa wanapendelea sana magari manual kwa sababu hawakai kwenye mafoleni sana. na pia ni rahisi kumaintain gear box ya manual kuliko ya auto maana ni less electronic.. na la msingi zaidi ni kwamba unasave mafuta zaidi kwa asilimia 3 au zaidi .... na mwisho kabisa kwa dereva anayependa kuendesha manual transimision ina raha zaidi ya auto.

    ReplyDelete
  14. Funny thing is wengi wanaosaga hawajawahi kuwa na gari,hawana uwezo wa kununua gari na hawajawahi kuwa na gari.

    ReplyDelete
  15. AnonymousJuly 09, 2010

    NI KWELI ULAYA HAWAPENDI SANA AUTOMATIC CARS, NDO MAANA HATA BEI AUTO NI CHEAP UKILINGANISHA NA MANUAL HATA SECOND HAND CARS MANUAL NI BEI ZAIDI YA AUTO.

    ReplyDelete
  16. AnonymousJuly 09, 2010

    820,000km ni kwamba imezunguka dunia zaidi ya mara 20

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...