ankal akiwa na Chacha Maginga wa TBC 1 (shoto) Bonny Luv, DJ Mackay na DJ Venture Mzalendo pub usiku wa kuamkia leo. Ankal ambaye hajafika siku nyingi kiasi kiota hiki cha maraha kinachowasha moto pale Kijitinyama Millenium Towers kila Jumamosi alibroo kukuta pamefurika wadau kibao toka kila pembe ya jiji na kwingineko. Wadau wanasema 'shimo la Mzalendo pub' limetapika. Yaani we acha tu. Ma Old Skul na madude ya Naija na kombe la dunia kama kawa. Pitia siku moja ujionee mwenyewe.
Ankal akutana pia na wadau damu wa Bwawa la Maini ambao wanasema baada ya kupatikana kwa kocha mpya basi vuvuzela mpaka lyamba ligi kuu ya Uingereza ikianza. Watani wa jadi kaeno chonjo. msimu huu twaja....

mzee wa konoz naona unaibeba liver ha haa haina shaka kama wewe umekubali basi lazima patakuwa pamekaa vizuri maana mi ni mdau mmoja wapo na huwa napenda sana waakina dada wanapozungusha mduara haaa
ReplyDeletekuna mkaka mmoja ilikua anaitwa bonny lov miaka ya tisini alisomea kagera nyakato sec school o.level ndio huyo DJ?swali kutoka kwa mdau wa mbali.
ReplyDeletehuyu bonny lov alisoma kagera?Nyakato sec school 0.level miaka ya tisini?
ReplyDelete