Katibu mkuu wa CCM Yusuf Makamba akimkaribisha Mwenyekiti wa CCM Taifa,Rais Jakaya Mrisho Kikwete katika ukumbi wa White House tayari kuongoza kikao cha kamati Kuu ya CCM mjini Dodoma leo asubuhi.
Mwenyekiti wa CCM Taifa ,Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongoza kikao cha Kamati kuu ya CCM mjini Dodoma leo asubuhi.Wengine waliokaa meza kuu kutoka kushoto ni Rais Mstaafu awamu ya Tatu Benjamin Mkapa, Rais Mstaafu awamu ya Pili ali Hassan Mwinyi, Rais wa Zanzibar Amani Abeid Karume,Katibu Mkuu wa CCM Yusuf Makamba, makamau mwenyekiti wa CCM Bara Pius Msekwa na Rais Mstaafu wa Zanzibar Salmin Amour.
Wagombea Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM Makamu wa Rais Dr.Ali Mohamed Shein na Waziri kiongozi wa SMZ Shamsi Vuai Nahodha wakisalimiana katika viwanja vya makao Makuu ya CCM mjini Dodoma leo asubuhi. 



Ankal hivi hao ni wagombea urais wa Zanzibar au ni watu waliomba kuteuliwa na CCM ili wagombee urais wa Zanzibar???
ReplyDeleteHapo unanichanganya kuwaita ni wagombea uraisi
Sijuwi nimlaumu Freddy Maro au nani manake wote walioomba kugombea urais wa Zanzibar wanatambulishwa kama wagombea. Au mchakato umeshapita na sasa CCM itasimamisha wagombea watatu kwa mkupuo Zanzibar?
ReplyDeleteZANZIBAR INAWAGOMBEA WANGAPI WA CCM WA URAIS! HII NI MPYA! CUF WATASHINDA KWELI HAPO KAMA WAGOMBEA KIBAO WA CCM NA MMOJA WA CUF SI WATAAMBULIYA PATUPU HAPO!!!
ReplyDeleteVP atasaidia anaonekana si mtu anayehimiza kujitenga kama huyu jamaa wa sasa
ReplyDeletehttp://issamichuzi.blogspot.com/2009/11/nolndozzzz-saut-leo.html
ReplyDelete