Rais mstaafu wa awamu ya pili wa Tanzania Ali Hassan Mwinyi (katikati) akiongea na washiriki wa mkutano unaowahusisha marais wastaafu wa Afrika walioachia madaraka kwa njia ya amani leo jijini Dar es salaam. Kushoto kwake ni balozi Charles Stith ambaye pia ni mkurugenzi wa kuhifadhi kumbukumbu za marais wa Afrika.
Baadhi ya viongozi wastaafu wa nchi za Afrika na wale walioko madarakani wakifuatilia masuala mbalimbali wakati wa ufunguzi wa mkutano unaowahusisha marais wa Afrika walioachia madaraka kwa njia ya amani leo jijini Dar es salaam. Kutoka kushoto ni Rais mstaafu wa Jamuhuri ya Mauritius, Dkt. Kenneth Kaunda rais mstaafu wa Zambia, Waziri mkuu wa sasa wa Msumbiji Bi. Luisa Diogo na Waziri mkuu mstaafu wa Tanzania Fredrick Sumaye. Washiriki wa mkutano wa marais wastaafu wa Afrika walioachia madaraka kwa njia ya amani kutoka nchi mbalimbali za Afrika na vyuo vikuu kutoka ndani na nje ya Afrika wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zinawasilishwa wakati wa mkutano wa marais wa Afrika walioachia madaraka kwa njia ya amani leo jijini Dar es salaam.
(Picha na Aron Msigwa - Globu ya Jamii)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. Michuzi uwe unasema marais wa zamani mawaziri wa zamani sio Wastaafu.Kaunda alishindwa ktk Uchaguzi hakustaafu,Sumaye hakustaafu labda Mwinyi ndiye unaweza sema alistaafu ingawaje kipindi chake kilikwisha(kikatiba) kama isingekuwa hivyo angeendelea kuwepo madarakani.Kustaafu ni pale mtu anapoamua kibinafsi kuacha kazi maybe because of Afya,Umri au kuchoka kuwa madarakani/nyadhifa fulani.
    Huwa unaandika waziri mstaafu "fulani" wakati ukweli tunajua hakuteuliwa na Rais kuendelea kuwa waziri mfano Sumaye na wengine wengi.
    UNAPOTOSHA.

    ReplyDelete
  2. Mungu azidi kumpa afya tele Rais wetu mstaafu Mh. Mwinyi..(1925)
    Wamepishana only 3years na Baba wa taifa(1922)

    ReplyDelete
  3. anony wa kwanza: kisiasa 'kung'atuka' = kustaafu?
    wabunge wetu wana mikataba ya miaka mitano mitano, je hawaingii kwenye kundi la wastaafu wanapomali za mihula yao?

    ReplyDelete
  4. anony wa kwanza: kisiasa 'kung'atuka' = kustaafu?
    wabunge wetu wana mikataba ya miaka mitano mitano, je hawaingii kwenye kundi la wastaafu wanapomali za mihula yao?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...