Waganga wanafunzi kutoka chuo kikuu cha tiba cha Western Otawa cha nchini Canada wanaendesha zoezi la uchunguzi wa meno kwa wanafunzi wa darasa la kwanza na la pili katika shule ya msingi ya Themi ya mjini Arusha kwa kushirikiana na hospitali ya KAM ya mjini humo. Pichani ni mmoja ya waganga hao Chalice Valeriano akiandika maelezo baada ya kumfanyia uchunuguzi mmoja ya mwanafunzi.

Katika uchunguzi huo wa wanafunzi 180, karibu ama zaidi ya nusu yao, walibainika kuwa na matatizo ya mashimo katika meno na kushauriwa kwa yale meno ambayo bado ni ya utotoni yataondolewa na ambayo tayari yamekoma itafutwe tiba katika hospitali ya kuu ya serikali mkoani Arusha ya Mount Meru.

Kadhalika madaktari hao wanaunzi walitoa mafunzo ya upigaji wa mswaki na kutoa miswaki na dawa bure kwa wanafunzi hao ambao katika zoezi hilo waliandamana na wazazi wao.

Picha na habari na Novatus makunga

Mwalimu akimsaidia Chalice Valeriano maelezo ya mwanafunzi
Mzazi akipewa cheti cha matokeo ya
vipimo vya meno vya mwanae




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Sisi ndiyo kichwa cha mwendawazimu na kufanywa kama specimen za kufanyia field kwa wanafunzi wao kuona kama wamequalify. Wanajua hakuna risk ya litigation kama huko kwao. maana huko kila kitu ni mahakamani tu, ukimuokoa mtu aliyepata ajali na gari linaanza kuwaka na bahati mbaya wakati wa kumvuta akachubuka baadae akadevelop complecations kwenye mchubuko anakushitaki umlipe fidia kwa kumsababishia kilema cha maisha.

    ReplyDelete
  2. Wacha watufanye guinea piggy lakini just jiulize wewe check up ya meno ukiwa bongo ulifanyiwa lini? mtoto wangu just turned 3 yrs old na ameshamwona dentist mara mbili. Haya meno yataoza saa ngapi? Kwetu kumwona denstisty ni mpaka uwe unakwenda kutolewa jino..

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...