Mgombea Urais kwa tiketi ya CHADEMA Dk. Wilbroad Slaa akihutubia umati wa wakazi wa Mtwara alikoenda kutafuta udhamini sehemu ya umati mkubwa wa wakazi wa Mtwara mkutanoni hapo
Mmoja wa wanachama waandamizi wa CHADEMA
Bw. Saidi Arfi akisabahi wakazi wa Mtwara

Mh. Chiku Abwao akisalimia wakazi wa Mtwara.
Mh. Mabere Marando akiongea wakati wa mkutano huo
Picha zote ni kwa hisani ya mwana libeneke wa
Angalizo: Wadau wa libeneke popote pale mlipo tunaomba mtuletee picha za matukio haya na mengine huko mliko kupitia issamichuzi@gmail.com










Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 15 mpaka sasa

  1. Wish you all the best in the endeavor you have embarked on.

    Ushauri wa bwerere kwa Slaa;

    1. Hiyo ngoma ya ufisadi inaelekea kupasuka. Badilisheni

    2. Mkianza kupiga vita migodi mikubwa, mtapoteza wafanyakazi, familia na suppliers wengi wanaotegemea hii migodi

    3. Ongeleeni miundo mbinu.

    ReplyDelete
  2. Chenye Mwanzo huwa kina mwisho, hata wazungu walivyokuwa wanatusumbua wakati wa ukoloni hawakufikilia kama ipo siku hayo yote yataisha.. ule wakati wa wale waliotuibia fedha zetu na kuombwa kurudisha kwa kupewa siku kadhaa kama wafanyiwavyo wale ndugu zetu tunaish nao mtaan wakikwapua sim na kuishia miaka zaid ya mitano jela umefikia tamat.... umziken jaman mmetunyonya sana



    hata usipoweka ujumbe wanao masikion mwao

    ReplyDelete
  3. Michuzi unawaogopa sana wachaga wa Jamiiforums sio? toka walipokutisha kuwa hutoa habari za Dr Slaa sasa unabembeleza ulitewe picha. Acha zako hizo uwogo tu hawana lolote wachaga hao ukabila na udini kwa kwenda mbele amka!

    ReplyDelete
  4. Go ! Go ! Go ! Dk. Slaa

    Tumechoka na Ufisadi!! Tunaamini tutashinda , Mafisadi wamezidi kutafuna nnchi yetu.

    WaTz tunaweza,kwa pamoja tutashinda,wakati wa mabadiliko ni sasa.

    Hata USA hakuna aliyefikiri kuna siku itakuja kuongozwa na Mwafrika, lkn kwa pamoja wameweza.

    CHANGE - YES,WE CAN !!
    MADILIKO - NDIO, TUNAWEZA!!

    VIVA TANZANIA .VIVA DK SLAA!

    ReplyDelete
  5. Ushauri wa bure kwa Chadema: Hadi sasa chama chenu kinakwenda vizuri ila msikubali kuwapa watu uanachama bila uchunguzi wa kina, huyo Marando ameulizwa kadi ya CCM amerudisha lini? na funguo za ofisi "nyeti" alikabidhi lini. Yasije kuwakuta ya NCCR-Mageuzi!!

    ReplyDelete
  6. We anonn wa Thu Aug 05, 01:15:00 PM acha chuki zisizo na maana, nchi hii haina udini wala ukabila, Kama udini upo utasemaje ngazi za juu zote za uongozi wa Serikali wanaogombea bara na visiwani mwaka huu kupitia chama tawala, je huo ni Udini? angalia ngazi za kuteuliwa wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya, mabalozi na taasisi kadhaa, je huo ni UDINI?

    nchi hii haina UDINI wala ukabila Usichonganishe.

    ReplyDelete
  7. Aliyeimaliza TLP ameingia CHADEMA, mmemkaribisha mkilijua hilo. Tatizo la baadhi ya watu ni ukabila na Umajimbo, Chadema imekamatwa na Mangi, tutafika?

    Kalagabaho

    ReplyDelete
  8. CHANGE--------YES WE CAN!!!!!
    MABADILIKO---------NDIO TUNAWEZA!!!
    VIVAAA TANZANIA----VIVA DK.SLAA

    ReplyDelete
  9. Hivi kuuliza si ujunga jamani,kwanini? CHADEMA kumejazana sana wachaga? na pia inaonekana hawana sela wa hoja ya msingi ya kuwavuta watu heti sura mpya,yaani ndio kusema watanzania wanahitaji sura mpya?

    ReplyDelete
  10. Mabere ni 'opportunist' CHADEMA msingepokea hicho 'kimeo cha kufa mtu'!!

    ReplyDelete
  11. nyie mnaosema wachaga acheni uchonganishi, hakuna ukabila wala udini kwenye chama kama hivyo basi tuseme serikali ya kikwete maana ameweka waislam kibao na maswhiba wake, inamaana ccm ni ya waislam.

    ReplyDelete
  12. Anony wa Thu Aug 05, 08:16:00 PM

    Mbowe - Mchaga wa Hai
    Zitto Kabwe - Muha
    Mabere Marando- Mjaluo
    Rwakatale- Mhaya

    Au nimekosea?


    Nkyabo - Bongo

    ReplyDelete
  13. BILA CHALLENGE NCHI HAIWEZI KUENDELEA! WAPENI NAFASI DEMOCRASY JAMANI, MIAKA MINNE TU! KAMA WATASHINDWA SI MTARUDI KWENYE MAPINDUZI.
    HALAFU PALE MAPINDUZI WATAPOKAA BENCHI MIAKA MINNE, NDIO WATAAMKA, WATAJIFUNZA NA WATAMUHESHIMU MTANZANIA NA TANZANIA.
    KAMA NCHI NYINGINE ZOTE ZA MAENDELEO. ANGALIENI GHANA TU WENZENU EH!
    WACHENI UOGA WABONGO KWENYE MAENDELEO NA UNAPOTAKA KUPIGANIA HAKI YAKO.
    NCHI INATAWALIWA NA CHAMA KIMOJA TU TOKEA NCHI IZALIWE DUH!

    ReplyDelete
  14. Wee An. wa Thu Aug 05, 01:15:00 PM, kumbuka kuwa Jamiiforums ni mali ya Mhaya aitwaye Max Melo. Wachangiaji wakubwa wa kule ni Mwanakijiji ambaye kuna tetesi anatoka Mbeya. Sasa Michuzi kaogopa vipi tena JF? Kwenye Mafuriko alikuwa ni mmoja wetu kwenye kuchangia waliopatwa na Mafuriko.

    Michuzi, huwa unaniuwa pale unapotoa jumbe za watu nzimanzima wakikulaani. Kwa hili naona unacheza fair play kwa saana. Libeneke oyeee ankal Mithupu.

    Kusema ukweli hata mie mwanzo nilikuwa na wasiwasi ila kwa sasa nina imani kuwa Michuzi utacheza FAIR PLAY kwa wagombeaji wote wa uchaguzi Mkuu Tanzania hasa ngazi ya URAIS. Nina imani Chadema na CUF pamoja na wagombeaji wengine wa Urais, wataleta habari na picha zao. Ila pia jitahidi LIBENEKE lako pia lizitafute taswira nyingine maana wengine wanatumia kamera za simu na wewe Ankal nafahamu lile D5 lako likitema mwanga basi picha hiyo una hakika ni nzuri. Again, Libeneke Oyee. Mdau wako Sizya.

    ReplyDelete
  15. Wee Anon wa Tarehe Thu Aug 05, 02:10:00 PM

    Go ! Go ! Go ! Dk. Yes I agree!!Go Go Go where? To political oblivion in the annals of history. Mmemmaliza padre wa watu. Siasa kweli mchezo mchafu. Go goo

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...