Mmoja wa marehemu, Omar Ali Jadi

Wagombea wawili katika uchaguzi mkuu ujao wa nafasi za uwakilishi na udiwani kupitia chama cha wananchi CUF wamefariki dunia usiku wa kumkia leo.

Akizungumza na Zenji fm radio mkurugenzi wa mawasiliano ya umma CUF Salum Bimani amesema waliofariki ni mgombea wa nafasi ya uwakilishi jimbo la Kojani Omar Ali Jadi.

Amesema Jadi ambae ni mwakilishi wa zamani wa Jimbo hilo amefariki dunia katika hospitali ya Chakechake Pemba.

Bimani amemtaja mgombea mwengine aliefariki dunia katika nafasi ya udiwani wadi ya Kikwajuni ni Shani Ahmad Shani. Amesema mgombea huyo amefariki dunia kwa ajali ya gari alipokuwa akirejesha fomu za kugombea nafasi hiyo.

Bimani ameiambia Zenji Fm radio kuwa CUF inawasiliana na tume ya uchaguzi Zanzibar ili kupeleka majina mengine ya wanachama wao watakaogombea nafasi hizo

Source: http://zanzibarislamicnews.wordpress.com/

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...