Mr. Michuzi,
Bado unazunguka kwenye kampeni?
Mie nipo Dodoma na baadae Morogoro kesho, ila mwisho wa wiki ijayo nitaondoka. Kaka wajanja karibia wanilize kweli, na nimepata hasara kubwa sana.

Kuna mtu aliniagizia vitu vya bei kweli, yaani ghali mno, na baada ya kufika akataka nimpe alafu alete hela baada ya siku mbili, kumbe hakuwa hata na senti tano.

Sasa mimi nikamwambia aje na hela baada ya siku mbili avichukue hivyo vitu vyake lakini aliporudi ikawa ni viswahili vingi kama kawaida baada ya kuniingiza kwenye hasara ya $5,900 na huyu ni mtoto wa wanaoitafuna hii nchi. Hii saa ni moja ya vitu nilivyomletea na ndiyo ya mwisho, vingine vyote imenibidi nigawe tu.

Niliinunua $1,050 ila nalazimika kuiuza chini na ambayo sina hata uhakika nitaipata. Naomba niweke hii kwenye blog ya jamii


LUXURY WATCH FOR SALE
State of the Art, Fully Automatic Luxury, Eco Drive Men's Leather Watch, is up for a grab.This is a brand new model (watch) that functions automatically, does not need a BATTERY replacement and can store energy for over 300 days. IT is fully automatic and one of the best money can buy. $799 or best offer

For questions contact mbezi1980@yahoo.com or 0713-842-329

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 33 mpaka sasa

  1. Wewe ndio mjanja wa mjini unayetaka kutuuzia saa kwa maneno mareeeefu. Wala hakuna mtu aliyetaka kukuingiza mjini, wala nini. Hiyo ni gia yako tu ya kutangaza saa.

    Hata kama Bill Gates atanunua hiyo saa, mimi naona yatakuwa matumizi mabaya ya pesa zake. Saa nzuri zaidi na ya bei rahisi inapatikana.

    ReplyDelete
  2. Next time akili kichwani.
    Wabongo ni wataka makubwa lakini hawana pesa.wanapenda sana kuwa take advantage watu wanoishi nje.Atleast vitu unavyo.Lasivyo ungepigwa chenga mpaka siku ya kuondoka.

    ReplyDelete
  3. Sio mchina hiyo dogo?mmmmmmmm?

    ReplyDelete
  4. Unaleta UTANI na USD 799...what? that kind of watch for that money..wizi mtupu..u deserve kutapeliwa..or we tapeli nini..go visit.
    http://www.nextag.com/citizen-mens-eco_-_drive-leather-watch/compare-html

    ReplyDelete
  5. sorry ila wewe ni mpumbavu aisee,sinunui hiyo saa juu ya dola 200 aisee tena hapo nimekuonea huruma na tena iwe ya ukweli sio mambo ya china aisee,wakamate wabongo huko africa hao ndio mang'ombe utawakamua tu,siku njema ila usirudie tena aisee.

    ReplyDelete
  6. Do you think us Tanzanians are STUPID? Wewe tapeli tuu. See http://www.citizenwatch.com/COA/English/detail.asp?Country=COA&Language=English&ModelNumber=AT0910-00E

    This watch is Model AT0910-00E inapatikana kwa $295 before discount!!

    Think Again,

    Mdau
    Ndanda, Ntwara.

    ReplyDelete
  7. duh pole sana mkuu kama kweli jamaa alikuagiza hivi vitu,nakumbuka ulitangaza pia ipad.wabongo usiamini kupeleka kitu kabla hajalipa advance.

    ReplyDelete
  8. Duh, kweli,bongo usanii, kaanza kwa hadith ndeefu utadhani kweli, afu anataka ingiza watu mkenge, saa hiyo hiyo (rangi,materials na brand name) ni dola &210, weka na usafirishaji haizidi $300.

    Aseme anatafuta ticket ya kurudia si kudanganya watu.

    Nenda www.amazon.com uhakikishe mwenyewe.

    Mdau
    Sweden

    ReplyDelete
  9. Maelezo yako hayana kichwa wala miguu, inaonyesha hujui hata kutoa maelezo ya kitu ulichonacho sana sana unaongea neno automatic tu as if umetoka kulijua jana, huelezei functionalities zake unaishia kusema ni fully automatic, tueleze inaautomate functions zipi. After all, japo Watanzania wengi ni wapuuzi ila hakuna atakayefikia kununua hiyo saa kwa zaidi ya milioni moja. Saa ya nini wakati siku hizi kila sehemu kuna saa. watu wanamiliki simu tatu tatu, zote zina saa, computer zina saa, magari yana saa, Tv zina saa, radio zina saa hata minara barabarani ina saa. Huo ni mzigo tu, kwa kukusaidia saaaaana mimi ntanunua kwa buku 3 ili nimwachie mwanangu achezee.

    ReplyDelete
  10. Ni nzuri sana, lakini duka lenyewe tu, ikisinzia nikutafute kwenye yahoo.com? anuani ya makazi ya kudumu, sio hoteli ni nzuri zaidi angalau hata kama nisipokupata naweza nikang'a kadirisha kufidia hasara.

    ReplyDelete
  11. Kaka acha usanii hiyo saa haiwezi kufika $1000 mie ninayo kama hiyo nimenunua kwa $300 sasa unauza $700 ndio punguzo mh!!! huo ni utapeli ama kweli bongo siku hizi matapeli kinoma utafikiri tuko nigeria!!!

    ReplyDelete
  12. Umeshagawa $ 5000 nzima hiyo dola 1000 unashindwa nini kumalizia kuigawa!!!Natania tu.

    ReplyDelete
  13. Acha usanii wewe,Misupu itabidi akulipe huyu kwa matangazo.

    ReplyDelete
  14. yaani hii saa sijui kama inavalika maana mbona makorokoro mengi?ipo complicated sana!ila kila la kheri watajitokeza watakayoipenda ila kuwa makini na wasanii wasije wakakuzuga kama huyo wa awali!

    ReplyDelete
  15. nshimimana aka dumisaneSeptember 23, 2010

    Mbezi 1980, sasa nitakupataje? do you ship to U.S. ?

    nimekuwa nakifukuzia sana hiki chombo, kweli mimi nina bahati.

    anyway.

    nitakupigia, tuongee.

    = = =
    Buffalo,
    New York

    ReplyDelete
  16. Wewe kama unauza kitu just hit it straight no one want to hear those mambo jambo or yari yarie. Too much information is unnessary au ndo kama kawaida yako kinda of showing off huh?
    Mdau Bariadi

    ReplyDelete
  17. wewe john mashaka acha ushamba kwa nini usirudi nayo uiweke kwenye ebay hapo Bongo watu wamechoka hiyo asking price yako trust me you will never get it labda ingekua I-fone au Blackberry ndo wangenunua si unajua wabongo tunajulikana duniani for Talking big but walking small
    Mdau Silver Spring (discover Chanel BLDG)

    ReplyDelete
  18. Sasa wewe unataka kutapeli. Hizo saa hazizidi $150 amazon.com

    ReplyDelete
  19. hivi ni biashara gani mnayoifanya badala ya kufanya vitu vya maana mnaendekeza nini sasa? kumbukeni kuna watu hapa hapa tanzania wanakufa na njaa hawanachakula nyie mnafanya nini hii sasa ? kuweni wastaarabu na waungwana mungu hapendezewi na kufuru mnazofanya sas hiyo saa ndio yakununua kwa pesa zote hiyo ? au ukivaa ndio haufi?

    ReplyDelete
  20. john mashaka pole sana wabongo ndo zao wanapenda kulalia sana, ukianza kudai linazuka bonge la ugomvi yani usanii mwingi mno next time usilete kitu hata iweje utalizwa bureeee!!!je ankal umeipenda nikupige present ya ukweli?

    ReplyDelete
  21. Pole sana John Mashaka.

    Ndio maisha.

    ReplyDelete
  22. Huyu Bwana tapeli. Kwanini andanganya watu kwa kusingizia wanaotafuna nchi kumbe yeye ataka kuwatafuna wengine! Saa hiyo hata ukiende kwenye website ya COSTCO utaiona kwa dola $115. Yaani karibu laki moja sabini! Nchi yetu kila mtu anajaribu kumla mwingine!!!

    ReplyDelete
  23. uda mwengine haina haja kuanza Kuongelea Historia nzima wewe sema tu unaiuza basi kuhusu huyo mtu mwengine haina haja kumzalilisha binadamu mwenzako ndomana kila kitu kina majaliwa ya mwenyezimungu, Mungu atakusaidia utapata mteja mpya.

    ReplyDelete
  24. Ebo!! Huyu jamaa kanitoa tongox2, tangu nimezaliwa maeneo ya Bukoba miaka 27 iliyopita sijawahi kuona saa ya bei kubwa kiasi hii, au ni ushamba wangu? Ila inaonekana leather yake ni kiboko.


    Nkyabo - Bongo

    ReplyDelete
  25. MZEE WA MBEZI SI USEME TU KAMA UMECHACHA NA UNAUZA SAA YAKO? KAMA HIVYO VINGINE ULIGAWA KWA NINI NA HIYO USIGAWE?? KAMA ULIWEZA KUGAWA VITU VYA THAMANI ZAIDI YA DOLLAR 4000 KWA NINI HIYO YA DOLLAR 1000 USHINDWE???? WACHA UJANJA MZEE WA MBEZI WABONGO SIKU HIZI TUMEAMKA....

    ReplyDelete
  26. nA HIYO TOA KAMA ZAWADI AU TUNZA TU KUNA SIKU ITAKUSAIDA KUANGALIA MAJIRA!

    ReplyDelete
  27. wewe acha wizi yaani dunia hii matapeli mpaka kwenye Michuzi Blog.
    Hiyo saa kwanza inaweza kuwa fake pili bei uliyotaja labda ndani waweke diamond. Bei yake hapa ukerewe ni £189 na nasema hivyo sababu hiyo saa mimi nimenunua na ukiongeza £18 unapata extra three year warrant ontop oif two manufacture warrant nenda migodini huko ukawaibie siyo hapa mjini.
    Huoni hata aibu mpaka namba ya simu unaweka tapeli mkubwa

    mdau ukerewe

    ReplyDelete
  28. Yaani brother mie ninayo saa kama hii nilinunua pale Washington DC mwaka juzi kwa USD 899,hiyo bei ni ndogo sana yaani nakutafuta sasa hivi nimpelekee house boy wangu.

    ReplyDelete
  29. That is a non-sense ever advertisement ever seen in my entire life. Kaka Michuzi hebu zingatia masuala muhimu yanayohusu "Future" ya Tanzania na sio huu upuuzi wa bling-bling. Unajua mwenyewe tumetoka mbali, tangia enzi za "MIDO"- Mission Quartet.

    ReplyDelete
  30. hivi we jamaa una akili kweli! wewe unafikiri mtanzania na ujinga wake anaweza kununua saa kwa sh milioni moja ina nini cha zaid au ina hotel ndani?mjomba hiyo utapiganayo picha tu

    ReplyDelete
  31. SAA ZIKO MPAKA ZA DOLA 3000 WATU WANANUNUA,ZINA WARANTY RISITI YENYE DETAIS ZAKO ILI UIWEKEE INSURANCE NA IKIWA NA TATATIZI UNAWEZA KUIPELEKA KWA DELAR YOYOTE DUNUANI.BADO NAKUMBUKA 1997 WAKATI RADO ZA MCHINA ZINAINGIA ZIEUZWA SANA SALAMANDER TSH 500.000.BUT THIS IS 21 MILLENIUM BRO.

    ReplyDelete
  32. Acha kutupiga changa la macho embu angalia bei yake http://compare.ebay.com/like/170537554875?ltyp=AllFixedPriceItemTypes&var=sbar
    US $162.
    wizi mtupu!na wewe kaka michuzi usikubali matangazo ya kitapeli kwenye blog yako, Usijiharibie uaminifu wako

    ReplyDelete
  33. wadau wadau msibeke ovyo zameni google muanalie bei ya rolex, haki ya nani unanunua kiwanja sinza lo lo loooo!!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...