Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza katika kikao cha kujadili maendeleo ya Millenia alichokiandaa kwa pamoja na Waziri Mkuu wa Denmark, L. Lokke Rasmussen (katikati) na Rais wa Liberia, E. Johnson Sirleaf jijini New York , Septemba 22, 2010.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza katika kikao cha kujadili maendeleo ya Millenia alichokiandaa kwa pamoja na Waziri Mkuu wa Denmark, L. Lokke Rasmussen (kulia) na Rais wa Liberia, E. Johnson Sirleaf (katikati) jijini New York , Septemba 22, 2010.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na Rais wa Liberia, E. Johnson Sirleaf (katikati) wakizungumza na Waziri Mkuu wa Denmark, L. Lokke Rasmusen baada y kikao walichokiandaa cha kujadili maendeleo ya Millenia kilichofanyika jijini New York Septemba 22, 2010
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri, New York, Robert Rimbo kabla ya mazungumzo yao kwenye hoteli ya Intercontinental jijini New York.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. Unajua ukivaa kanzu kuna taratibu zake, Ukivaa mgorori nao una taratibu zake,za kimasai nazo zina utaratibu wake... Kila vazi lina utaratibu wake kasoro wewe ukiwa msanii au mtu wa shoo unatengeneze sahihi yako.(signature yako) hivyo hufuati utaratibu maana unajiuza na unataka watu wakufuate wewe na ndio mafanikio yako yanakuja.

    Sasa Mzee Pinda yeye ni PM wa Tanzania hivyo hana choice ya peke yake kuwa anaweza kuavaa tu anavyotaka. sasa naona mambo ya kufunga vifungo vya koti unavyokuwa umesimama, unatembea yeye hajali matokeoa yake anaonekana kama Bitozi .....na sio PM wa watu milioni40+ matokeo yake wenyeji watamuona hayupo serious ama mbabaishaji na hivyo Watanzania wote sisi ni wababaishaji.
    Wenzetu hukujaji kwa muono wa kwanza na unavyojiwakilisha(First Impression). Ukishaharibu hapo watu wanasema tu "next subject" maana wewe tayari.
    Ukiwaangalia hata Mr O akisimama tu anafunga vifungo vya koti then anakupa mkono ni utaratibu tu na hakuna choice ooooo mimi kivyangu vyangu.

    *******Tatizo hii bulogu ya Ankal imekuwa kama "UBAO TU WA MATANGAZO" hivyo hata debate ngumu vikiandikwa tu ukichelewa kiduchu tayari ashafuta....hivyo ile maana halisi ya Bulogu watu watoe mawazo yao mbalimbali kwa uhuru inakuwa imepotea. Pengine ataufanyia kazi iwe tofauti*******
    Mzawa

    ReplyDelete
  2. Saidia baba!

    ReplyDelete
  3. tatizo letu sie watanzania tunajua na kupenda sana kukosoa bila kuwa na facts au uchambuzi wa kina wa issues mbalimbali.
    huyu bwana aliyemkosoa mzee wetu PM ina maana hajamuona huyo waziri mkuu wa DENMARK kuwa naye hajafunga hilo koti kama anvyosema yeye kuwa inaonyesha u seriousness.
    cha ajabu ni kipi katika hilo??? kufunga vifungo vya koti au yale anayoyaongea na waheshimiwa wenzake??? tuache kuendekeza uzungu ambao wakati mwingine hauna hata maana kwetu.lets try and be positive kwa viongozi wetu
    NAOMBA KUWASILISHA

    ReplyDelete
  4. Nimependa staili ya mama Liberia ya kuutangaza uafrika wake. Waliberia wana asili ya umarekani hivo walishachoshwa na kuiga uzungu sasa imebaki kula mila zao.

    Watu wasije kusema kufunika nywele ni kama dini ile takatifu, hapana, asili ya mwanadamu (hata sisi afrika) mama zetu hufunika nyele kwa stara.

    Uzuri wa mwanamke ni alvyo siyo nywele.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...