Ankal pole kazi
Naomba kuuliza. Hivi hii sehemu ya barabara service road inamaanisha ku-service vimeo ama vipi. Mfano huyu jamaa ndo kageuza garage hapo. Naomba kugahamishwa
Sent from my BlackBerry® smartphone from Vodacom

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 18 mpaka sasa

  1. ANKAL MICHUZI WEKA HII ILI KUMSAIDIA HUYU MDAU MWENZETU.

    KWANZA HAYA MBONA MAMBO MADOGO SANA KWA TANZANIA. TUNATAKIWA KUPAMBANA NA CHANZO SIO MATOKEA. HAPA HAKUNA MTU ANAFUATILIA KWA MAANA YA VIONGOZI WANAOHUSIKA NA MATUMIZI YA BARABARA. NA WAO HAWAFUATILII KWA SABABU HAWAFUATILIWI NA WAKUBWA WAO. WAKUBWA WAO UNAWEZA KUWAFUATILIA NA KUWAJUA MWENYEWE. UKISHAWAJUA SASA UJIUZE AU UWAULIZE KWANI NINI HAWAFUATILII HII KERO. KAMA ITAKUWA KWA SABABU YA UZEMBE, JIULIZE NANI ALIWAPA WATU WAZEMBE KAZI. NADHANI MWISHO KABISA UTAGUNDUA NI WAPIGA KURA NA WEWE UKIWA MMOJA WAO NDIYO WALIWAPA KAZI KWA MKATABA WA KIPINDI CHA MIAKA MITANO. KWA BAHATI NZURI AU MBAYA MIAKA MITANO MWISHO WAKE NI MWEZI HUU, SASA FIKIRI WEWE NA WAPIGA KURA WENZAKO KAMA UTAWAPA TENA MIAKA MITANO IJAO WAKATI WAMESHINDWA KUSIMIMIA SERVICE ROAD.

    NCHI ZENYE VIONGOZI MAKINI KILA KITU KINAENDESHWA KWA KUFUATA SHERIA NA KANUNI. NA VIONGOZI WANAHAKIKISHA SHERIA NA KANUNI HIZO ZIPO NA ZINAFUATWA. NA WANANCHI WOTE WANAELEWA HIVYO.

    ReplyDelete
  2. hivi kweli inaitwa barabara ya bandela road ? wabongo bwana ....

    ReplyDelete
  3. Sasa Michuzi, barabara ya Morogoro Road ndio nini?

    ReplyDelete
  4. bongo tambarare...wewe ulitaka hilo gari alibebe kichwani kulipeleka garage?

    ReplyDelete
  5. Huwaga mpaka wanashusha injini hapo hapo...mbona hiyo ni kawaida tu! Kwa Bongo yetu, sheria zipo lakini hazifanyi kazi kabisa.

    ReplyDelete
  6. Wat wld you do kama ni wewe ? hiyo gari unaona ni mbovu halafu ina mzigo how do you take it to the garage au unaongea tu ...? ingekuwa gari ndogo sawa unaweza kuivuta but not such a truck at such circumstances. let the dude fix his truck aondoke zake may be he went kuchukua spare parts ! wait he comes back fix and go deliver the cargo !

    ReplyDelete
  7. Kabla ya kumjulisha Michuzi bila shaka pia umewajulisha afande Mwema na Kova kupitia simu jamii, kama hujafanya hivyo nakushauri uwajulishe.

    ReplyDelete
  8. siyo garage tu, je na vile vipande vipande vilivyoachwa vinavyo uwa mataili ya magari yetu. inamaana jamaa hawajalipwa ndo wamegoma au kazi ndo imeisha?

    By
    The 2015 Minister of Science and Technology.

    ReplyDelete
  9. Kamanda Mohamed Mpinga
    Hali hii imeshamiri sana Barabara ya Mandela, yaani imekuwa kero tena kero sana, zaidi nashangaa kuona Mkandarasi hakuweka njia ya kuchepuka magari yanayotoka Buguruni kuelekea Tabata kwani kubaki kwenye foleni wakati yangeweza kuchepuka na kupita ni tatizo la kiufundi sana. Pia nafikiri pale Tabata Dampo panatakiwa kufumuliwa upya kwani barabara inayotoka Kigogo inapitia wapi kuingia barabara kuu. Halafu Mkandarasi wa Barabara ya Mandela ni mharibifu wa makusudi wa magari yetu ya ngama, barabara anaicha na viporo vinavyoumiza sana magari. Hivi Mhandisi Mkazi yuko wapi?? Hizi BODI zilizopo mbona mmelalal au nanyi mpo kwenye mchakato wa Uchaguzi???

    ReplyDelete
  10. Jamani Lugha NI KAAZ KWELI KWELI.

    1. service road barabara ya mandela road

    2. huduma ya barabara ya Barabara ya Mandela Road

    3. huduma ya barabara ya Barabara ya Mandela barabara

    ReplyDelete
  11. Hivi maana ya service road ni nini? Nilidhani hii ndiyo kazi yake hasa na sio kupitisha madereva wanaotanua na kukatisha foleni!

    ReplyDelete
  12. BONGO SHERIA ZIPO LIKIZONI,KUNZ FUNUNU ZITAREJEA BAADA YA MIONGO KAZAA.

    MDAU

    ReplyDelete
  13. Kama ktu hujui uliza sio ku post vitu usivyovijua. Ngoma ikisha lamba lumbesa kwa sheria za TRA gari haliruhusiwi kutoka nje ya Mandela Rd

    Ni kosa la jinai. Na migari spare za china lazima ziharibike na pahala pa kutengezea ndio hivyo tena.

    ReplyDelete
  14. CHANGAMOTO: ASILIMIA KUBWA YA AJALI ZA BARABARANI LAZIMA UTAKUTA KUNA ROLI LINAHUSIKA...AIDHA LIMEHARIBIKA NJIANI,MLIMANI AU LINAOVERTAKE, NA KUSABABISHA AJALI. HEBU VIJANA WA KOVA IFANYIENI RESEARCH HII NA MNAWEZA KUJA NA SOLUTION MOJAWAPO KTK KUPUNGUZA ALALI TZ.
    BHUBA.

    ReplyDelete
  15. Service road = a local road that runs parallel to an expressway and allows local traffic to gain access to property

    ReplyDelete
  16. We acha u,pita buguruni sehemu inaitwa wahenga- ni balaa kweli pesa ni sabuni ya roho Tz

    ReplyDelete
  17. annoy unayesema whay would you do kama ina mizigo...Wee ndio huelewi. Hoyo kari haikuharibiakia hapo bal i ilipelekwa hapo kwa kuengenezwa. hapo ni kama mini car repair shop. Hii hata mimi najiuliza wenye sheria wako wapi? Hawaoni hii kitu na hata magari yao unaweza kuyaona humo

    ReplyDelete
  18. hao jamaa walioharibikiwa walitakiwa waite tow truck ichukue hicho kichwa kibovu na kukipeleka garage kwa matengenezo. baada ya hapo inatakiwa kiitwe kichwa kingine kichukue huo mzigo na kupeleka kunakohusika. nategemea huo mzigo ulitakiwa ufike kunapohusika ktk muda maalum uliopangwa.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...