Hapa ni Chake Chake, Pemba, ambako taswira yake inaenda ikibadilika kila siku kwa majengo mapya pamoja na miundombinu ikiwa ni pamoja na umeme wa uhakika toka katika gridi ya Taifa kupitia Tanga. Pia watu wa Pemba ni wakarimu na wacheshi, jambo ambalo limeongezeka maradufu baada ya muafaka kukamilika na makubaliano ya serikali ya mseto visiwani kupotishwa kwa kauli moja. Leo hii wakati kampeni zinaendelea Pemba iko poa na kila mtu anashabikia chama anachokitaka bila kelele wala mikwaruzo kama ilivyokuwa awali kabla ya muafaka.
Ni majira ya mchana ambapo vijana wengine wanatoka Darsa na wengine wakielekea skuli kwa furaha na utulivu ambavyo ni asili ya visiwani humu

Majengo ya kisasa yanachipua kila kona ya Pemba sasa
Nidhamu mahotelini kama kawa....
Ng'ombe ni mojawapo ya njia kuu za kusafirisha bidhaa
Chake Chake ya leo
Rutuba kwa wingi Pemba kiasi kwamba inafanana na Tukuyu, Moshi ama Bukoba kwa mazao na hali ya hewa pamoja na ukijani usio wa kawaida kwa sehemu ya pwani Vespa ni usafiri muhimu kisiwani Pemba
Mtangazaji mahiri wa TBC 1 wa Songea, mdau Gerson Msigwa, akifurahia mandhari Pemba









Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 30 mpaka sasa

  1. Sijui niseme hizi picha zinanikumbusha ile movie ya "Time travellers" au "Going back in time"? Nakumbuka zamani(mwanzo wa miaka ya 80) palikuwa na kitabu cha Atlas kinaonyesha picha za Pemba na Unguja zilikuwa hivi hivi.Yaani hapa nina raha tupu.

    ReplyDelete
  2. kuna picha zimenikumbusha picha za kule Afghanstan!!kumbe pemba ndivyo kulivyo

    ReplyDelete
  3. Hizo Burqa..... Asante Michuzi maana nilikuwa katika mchakato wa kutembelea Pemba lakini burqa sijawahi vaa... inakuwaje hapo au ndio bakora!

    ReplyDelete
  4. Safi sana pemba inaanza kujengwa upya hureee. Wana Mbagala wenye asili ya Pemba twende tukalete maendeleo yumbani tukajenge mji wetu. Kidumu....

    ReplyDelete
  5. Michuzi huna lolote, hii najua ni moja ya kampeni zako za CCM...
    Tutolee hapa

    ReplyDelete
  6. Mh! Kwenye hiyo hoteli hapo Mgombea wetu hawezi kuingia na Mchumba wake! Habari ndio hiyo!

    ReplyDelete
  7. mgombea wenu nani hawezi ingia na mchumba? bora hata mchumba mana anaweza kumuoa kuliko kupokonya mke wa mtu ovyoooooooooo janaume zimaaaaaaa

    ReplyDelete
  8. Mtowa maoni wa tatu una akili finyu sana. Akili zako ni za kitoto sana, huna la kufanya na maisha yako?

    Twaswira zote hizo hujaona kitu ila burqa! Umjinga kiasi gani wewe? Hukufika pemba na wala usifike huzidishi wala hupunguzi.!

    Nani anataka watu wenye mentality kama zako?

    ReplyDelete
  9. mdau #3 juu
    na ngoja CUF wachukue nchi adabu zitawashika na mtazoea kuvaa tu kama mnavovaa vichupi ughaibuni

    visiwa mwanana sana ivi

    ReplyDelete
  10. hivi huwezi kuwa mwislamu bila vaa hayo ma scupy burka hayo niliona waafghanistani/ wataleban wanawalazimisha wanawake zao kujigubika kisa wasipovaa watwatia mshawasha

    ReplyDelete
  11. Kuna mtu mmoja ameshtukia hapa kama hivi ni kampeni tu za kuitangaza CCM Hata mimi nimefahamuy moja kwa moja ila mwenzangu ameshanitangulia.
    Haya hata wakifanya nini pemba hawapati kitu,Pemba haina hata waziri mmoja,pemba haina hata wizara moja,hadi wakuu wa mikoa wanakaa Unguja je kutakua namaendeleo gani,Nyumba ya ghorofa pema ndio hizo mbili mloziona tu.

    ReplyDelete
  12. Bongo mtakomaaa wapemba wote wameamua kujenga kwao sasa!

    ReplyDelete
  13. Mdau usinikasirikie bure, mie nimesema kulingana na hizo sheria za hoteli, mgombea wetu hawezi kuingia humo na mchumba wake hata kama ni mke wa mtu haijalishi sisi tunajua ni mchumba wake maana hajamuoa bado ingawa zamani alikuwa kimada wake. Kwa hiyo narudia tena mgombea wetu hawezi kuingia hiyo hoteli pemba!

    ReplyDelete
  14. Iko Siku Nitafika Pemba, Pemba Kuzuri Kunanukia Marashi Ya Karafuu, Walahi Pemba Nitafika...

    ReplyDelete
  15. sasa itakuaje hawa wanawake wakitaka kwenda ufaransa kwani huko serikali imepiga maruku full veil,wafaransa wanahofu kuwa wanawake wanalazimishwa kuvaa hayo mavazi na waume zao kama wanavyofanya watalebani

    ReplyDelete
  16. ingekuwa tunakwenda mbinguni kwa mavazi basi pemba 100% tayari wanadada hao wameshakata tiketi,Mungu awabariki wawe wasafi wa kiroho pia,mimi najiuliza utafahamuje jirani yako?

    ReplyDelete
  17. BASI PEMBA HAKUNA UKIMWI KWA MAZINGIRA HAYO!!!

    ReplyDelete
  18. mtoa mada wa saa 12:18 ungekaa kimya bila kuandika kitu ningekuona una busara kuliko kuandika vitu visivyoeleweka.

    Jifunze kuwa na adabu na imani za watu, xy nyoh !!!! zako

    ReplyDelete
  19. HILI TANGAZO LA HOTELI MMELIFAHAMU VIZURI HAPO HAKATAZWI MTU KUINGIA NA MSENGE WAKE KITU MUHIMU WAWE WAMEOWANA SASA SWALI LANGU KWANI PEMBA NDOA ZA NAMNA HIYO ZIMERUHUSIWA TAFADHALINI SOMENI VIZURI TANGAZO MIMI NAULIZA TU.
    KWA MAADILI YANAYODAIWA CHINI YA TANGAZO ITAKUWA AJABU KAMA NDOA ZA SAN FRANCISCO ZINATAMBULIWA CHAKE CHAKE.

    MAMA MIA.
    MWENGE GENGENI.

    ReplyDelete
  20. Tupigie picha na utundike baada ya matokeo ya uchaguzi kutangazwa ndipo utaijua Pemba halisi. Kwa sasa ni Pemba bandia.

    ReplyDelete
  21. anon wa Fri Oct 08, 12:18:00 PM uliambiwa na nani hayo? au nawe ni mmoja wa wale mbumbu wasiojua lolote na wakajifanya kuwa wanajuwa kila kitu?

    Umeambiwa na nani au kusoma katika kitabu gani za sheria za kiislamu kuwa huwi muislamu bila ya kuvaa burka kama ulivyosema hapa?

    Unajua ni nini burka? umeona wanaume wakivaa burka? jee una maana waislamu wakiume wote si waislamu kwa vile hawavai burka

    ReplyDelete
  22. Hata mimi sikujua Talibani wako pia Pemba. Na ngombe ndo chombo cha usafiri? waswahili bwana

    ReplyDelete
  23. BURGA IS A MOBILE PRISON?????au ni vazi la heshima kuwa mwanamke wa kiisilamu hapaswi kuonwa na mtu mwingine zaidi ya mumewe,naomba msaada wadau

    ReplyDelete
  24. kweli tembea uone tunashukuru hawa wakoloni walituletea dini za Mungu tofauti tofauti hiyo ndiyo pona yetu sisi wafuata dini za kigeni kwani laiti tungeletewa dini moja tu sijui wengine tungefanyaje TUNAVYPENDA MWANAMKE UNYWELE SIJUI TUNGEFANJE KWA HILI?

    ReplyDelete
  25. jamani acheni kumshambulia anony wa fri oct 08,12:18:00 PM mbona hajaongea kitu kibaya hapo ni ukweli kuwa watalebani,iran au saudi arabia mwanamke ni lazima kufunika kichwa tunaona kwenye tv kila siku na mwanamke atakayekiuka anapata adhabu ndio maana ameona bora aulize kwani huku bara haoni mambo kama hayo na kuna waisilamu wengi kuliko dini zingine?

    ReplyDelete
  26. Vyangu nifiche na hizo Bhurka visionekane na mwanamme mwingine ila wewe vyako uvitembeze kwa wanawake zaidi ya mmoja unaoruhusiwa kuoa. Kuna haki kweli?

    ReplyDelete
  27. Huwa hizo nguo nyeusi zinawekwa kwenye mikoba wakija bwawani kwenye muziki na kisha huzivaa wanaporejea kwao. Usiwaone hivyo ndani huvaa vichupi na visketi vifupi.Jimama moja jambazi liliweka SMG ndani walipovamia NBC ubungo Dar kabla ya kuingia gesti hiyo wakaguliwe ati

    ReplyDelete
  28. Tangazo lipo wazi na linaeleweka mwanaume aliyefunga ndoa na mwanaume mwenziwe ni ruksa, huko ni pemba kama mombasa vile. Wanaotoka nje ya pemba wanatakiwa wawe na uthibitisho wa ndoa hizo.

    ReplyDelete
  29. Duh , asante Ankal Mithupu kwa taswira hizi za Pemba.
    Pamebadilika sana , naona hata maghorofa ni mengi sana.Nimekaa hapo nikisimamia ujenzi wa kiwanda cha makonyo 1982-84.Ghorofa ndefu ilikuwa Machomanne na mimi nikikaa ghorofa ya tatu!
    Kweli ni kuzuri kama Tukyu na watu ni wema sana.
    Siasa ziliwatibua watu hawa.
    Na totoz vipi mbona hutuonyeshi?

    ReplyDelete
  30. Tanzania kuna uhuru wa mavazi. Ukitaka unaweza kuvaa burka usipotaka hulazimishwi. Naona kuna baadhi ya wachangiaji hapa juu wametoa comments ili wawatukane Waislamu na Uislamu na si kwa sababu nyingine. Lakini napenda kuwahakikishia : Sisi Waislamu tutaendelea kuweko Tanzania wasiopenda wakajitose jahanamu. Just get used to it: SISI WAISLAMU TANZANIA WE ARE GOING NOWHERE!!!! Wenye kutaka kuishi kwa heshima na sisi tutaishi nao kwa udugu, wenye kutuchukia hawatatufanya lolote ila chuki zao zitawaangamiza.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...