Mkurugenzi wa Kamati ya Miss Tanzania,Ankal Hashim Lundenga akiwa katika mazungumzo na wazazi wa Genevieve Emmanuel mrembo anaeiwakilisha Tanzania katika masindano ya Dunia,katika uwanja wa ndege wa J.K. Nyerere leo.

Ujumbe wa watu 5 ukiongozwa na Mkurugenzi wa Kamati ya Miss Tanzania bw. Hashim Lundenga umeondoka nchini leo kuelekea Sanya China katika kuhudhuria mashindano ya urembo ya dunia yaliyopangwa kufanyika Jumamosi Tarehe 30 Oktoba 2010.

Katika ujumbe huo yupo pia Katibu Mkuu wa Kamati bw. Bosco Majaliwa, Miss Tanzania Mshindi wa 2 Glory Mwanga, na Miss Temeke mshindi wa 2 Anna Daudi ambaye pia alifanikiwa kuingia katika 10 bora ya Fainali za Miss Tanzania 2010.

Mama Mzazi wa Miss Tanzania 2010 Genevieve Emmanuel, Mrs. Mary E. Mpangala pia yumo katika msafara huo ili kushuhudia Fainali hizo za kumtafuta Mrembo wa dunia ambazo zitafanyika Jumamosi hii katika kisiwa cha Hainan huko Sanya China.

Msafara huo unatarajia kurejea nchini Tarehe 3 Novemba 2010.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 16 mpaka sasa

  1. Duh! baba wa mrembo anaonekana akifikiria kwamba "laaaasalaleeee..... hii njemba ludenga siyo ya kuaminiwa hata kidogo na kabinti kangu...."

    ReplyDelete
  2. Dah wanarudi tarehe 3 Nov?!? Kwa hiyo hawatapiga kura!!! Safi sana!! Kura tano hizo CCM wamepoteza, ukichanganya na ya Miss Tanzania mwenyewe zinakuwa sita....!! Lazima wachakachuriwe mwaka huu!!!

    ReplyDelete
  3. tumesha wapoteza wapiga kula 5 tayali

    ReplyDelete
  4. hivi wanajuwa hao kwamba pengineo viongozi wanaowahitaji wawaongoze hawataweza kufanikiwa kwa kukosa kura zao? kura 5 zina maamuzi mazito ya nchi.

    ReplyDelete
  5. Badala ya kusema wanapoteza kura tano ni afazali mngesema namna itafutwe ili watanzania wanaojua watakuwa wamesafiri siku ya kupiga kura wapige kura mapema. Si muliona hata Bibi yake Obama alipiga kura mapema kisha akafarika siku chache kabla ya upigaji kura wa jumula?

    ReplyDelete
  6. Angalia jinsi ambavyo kamati ya miss tanzania haithamini haki za watanzania. kwanini wasiahirishe kwenda? kwani wao ndio majaji. kura zao ni muhimu sana kwa maendeleo ya taifa.

    ReplyDelete
  7. baba anaonekana kuhuzunika,kwani ni lazima aende jamani?mama alikuwa anatosha kumuwakilisha..tusi-false mambo jamani..

    ReplyDelete
  8. Janja ya nyani kwisa tambua,huyu Lundenga ni mjumbe wa yanga, na Huyu E. Mpangala halikadhalika. Hapa hatuwezi kupata mwakilishi halali Miss TZ. Unafiki mtupu, ni udugunization na urafikinization. Haya kashuhudieni nafasi ya 50.

    ReplyDelete
  9. Mwenyekiti Lundenga Mjumbe Yanga, E. Mpangala halikadhalika. Hapo mlichakachua mashindano. Na kwa kuwa mpangala ni kiwembe, sasa zamu yako.

    ReplyDelete
  10. Tunakutakia mafanikio Genevieve

    ReplyDelete
  11. Duu safi sanaaaa.... inaonekana Lundenga na Bosco wamagawana hawo ma-miss temeke na miss 2 wa tz, kila mmoja na demu wake hapo... kazi kweli kweli.

    ReplyDelete
  12. hapo lundenga anamawazo kwani anajua walichagua miss ambaye ni kiazi hana mvuto so anawaza jnsi watakavyo aibika

    ReplyDelete
  13. kwanza kabisa jamaa kashika tamaa kama anakwenda kutali pili anashukuru allowance wote hamna matumaini ya ushindi mpaka mwenyekiti wa kamatihuo ndo ushindi wa kujuana huwa unakosti

    ReplyDelete
  14. Hakuna lolote, hata huyo slaa mnaempigia debe ana tofauti gani na viongozi wengine waliopita au waliopo, yeye ndio ataibadilisha tanzania kirahisi, amekua Mungu?? wote binadamu, angalieni na mazuri aliyofanya JK, na waliotangulia, sio mnakalia vijembe visivyokua na maana,kuna mtu asiyependa pesa?? wewe hapo ukiambiwa sasa hivi unalishwa na kusomeshwa, unapewa nyumba, na magari ya kifahari au unapelekwa ulaya, utakataa?? wote wanochaguliwa wapo wanopenda mwaendeleo ya wananchi wao, na wapo wanaotaka madaraka kwa manufaa yao, kumbuka kuwa hata baba wa taifa alifanya mazuri mengi tu, lakini hata sasa kuna watu wanamponda, jifunzeni kushukuru,kubalini kuwa tanzania bado ni maskini, cha muhimu ni kuungana ili kutatua hayo matatizo, pia kumbuka kuwa teknolojia inabadilika, uchumi unapanda,kumbuka pia kuwa hiyo hiyo CCM ndio imekufikisha hapo ulipo, hii yote ni uoga tu kuaonyesha kwamba CCM hamuwawezi, KELELE ZA CHURA HIZOO!! TAHATS NOT POLOITICS! SAWA NA KELELE ZA DEBE TUPU!!

    ReplyDelete
  15. Ndahani hawatambui haki ya kimsingi na kikatiba.Kura tano nzima zinaenda kumwangali mrembo ambaye mpaka sasa she is out of top 40.

    ReplyDelete
  16. acheni hizo, nyie mnafikiria kura wakati wazee wazima wanaenda kujirusha na vimwana

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...