Mwenyekiti Danford Mpumilwa (shoto) akiwa na Katibualiyemaliza muda wake Kingdom Mwanguku hapo uwanjani.
Danford akiongozana na wanachama wenzakeDr. Weggoro na Mike Taylor wakikagua timu za watoto siku hiyo.
Mambo hayanogi bila vichombezo -Makamanda wa Oljoro wakiwa kazini.
Kamati mpya ilyochaguliwa siku hiyo.
Wapiga kura wakisikiliza kwa makinimaelezo ya upigaji kura.



Katika juhudi za kuendeleza michezo na undugu baina ya watu wa mataifa
mbalimbali waishio na kufanya kazi Arusha miaka kadhaa iliyopita
ilianzishwa timu moja ya michezo ya Arusha Wazee Sports Club.
Timu hiyo inayokua siku hadi siku ina wanachama zaidi ya 150 kutoka mataifa zaidi ya 20 ikiwemo Tanzania. Jumapili iliyopita wanachama wa timu hii walikutana kiwanjani kwao hapo General Tyre kufanya uchaguzi wao mkuu ambapo Danford Mpumilwa, mwanzilishi wa klabu hiyo, kwa mara nyingine tena alichaguliwa kuwa Mwenyeki ti wa Klabu hiyo ya watu wa enzi za Kifimbo. Wengine waliochaguliwa ni Makamu wake Aatsa Atogo toka Cameroon, Katibu; Ally Mamuya (Tanzania), Makamu wa Katibu; Saidou Guindo (Mali), Mtunza Fedha; Olomi (Tanzania), Naibu Mtunza Fedha; Ms Sophia Burra (Tanzania), Afisa Uhusiano; Emmanuel Ntoko (Cameroon), na Mwanasheria; Francis Kiwanga (Tanzania ).

Timu hii ambayo vilevile huendeleza vipaji vya watoto wadogo katika michezo
siku hiyo ilikaribisha timu mbili za watoto hao ambazo ni washirika wake za
Future Stars na Daraja Mbili zilizoonyesha ufundi wao. Burudani ilitolewa
na makamanda wa kikosi cha Jeshi la Kujenga Taifa la Oljoro ambako mkuu
wake Luteni Kanali Mmari ni mwanachama wa Wazee.

Sasa hivi Klabu ya Wazee iko mbioni kujenga nyumba ya klabu na viwanja vya
michezo hapo uwanja wa Nanenane mjini Arusha ambako itakuwa na makazi ya kudumu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. Nampongeza mpiga picha wetu.Inaonekana anajua kutunza "films za 1980s".Kwa muonekano hizi picha zinaashiria zimechukuliwa enzi za mwalimu wala sio jana.Samahani wakubwa ndo navyoziona.

    ReplyDelete
  2. Picha nzuri sana zinaonyesha hali ilivyokuwa enzi hizoooo wala sio hizi

    ReplyDelete
  3. Malafyale Danford, kwanza pole sana kwa kuukosa ule ubunge .Kukubali kushindwa ni uungwana.
    Nakutakia kila la heri na mafanikio kwa shughuli zako hapo AR.
    Nduguyo Malafyale Lawrence, POPOs Club-Bahari Beach

    ReplyDelete
  4. Danford "Lutengano". Nachoweza kusema ni "Long live Wazee Club". Eddy.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...