Mwenyekiti Tume ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania, Dk Fatma Mrisho akijiandaa kukata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa sura mpya ya kondomu ya Salama Studs, kushoto kwake ni Mkurugenzi Mtendaji wa PSI/Tanzania, Daniel Crapper.
Na Gaston Shayo
SHIRIKA linalotoa huduma na elimu ya afya nchini chini ya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, PSI/Tanzania limezindua sura mpya ya kondomu yake aina ya Salama Studs, maarufu kama Salama ya Vidutu.

Uzinduzi huo ulifanywa na Mwenyekiti mtendaji wa Tume ya Kudhibiti Ukimwi nchini (TACAIDS), Dk Fatma Mrisho jijini Dar es Salaam.

Akiongea katika uzinduzi huo, Dk Fatma alisema kuwa kondomu ni moja kinga zinazotegemewa sana katika mapambano dhidi ya kuenea kwa Virusi vya Ukimwi (VVU) hapa nchini na duniani kwa ujumla.

Alisema kuwa ugonjwa wa Ukimwi bado ni tishio na unaendela kuathiri maisha ya maelfu ya wananchi hivyo kutoa wito kwa Watanzania kuchukua hatua za makusudi kujilinda dhidi ya VVU.

Dk Fatma alisema alisema takwimu za kitfaifa zinaonyesha kuwa hali ya maambukizi ya kitaifa ni wastani wa asilimia 5.7, hii ikiwa ni kwa wanaume, na wanawake wenye umri kati ya miaka 15 hadi 49, kiwango ambacho alisema kuwa ni kikubwa kwa nchi kama Tanzania.

“Tunahitajika kuongeza mapambano na vita hii ngumu, kila mmoja wetu aweke dhamira ya kweli, ndiyo maana leo hii PSI TANZANIA mnapozindua muonekano mpya wa hii kondomu ya Salama, inaonyesha ni jinsi gani mlivyokuwa na dhamira ya kweli katika vita hii ngumu, hongereni,” alisema Dk. Fatma.

Alisema ziko njia nyingi za kuzuia maambukizi ya VVU na Ukimwi ikiwemo kuacha ngono na kuwa mwaminifu, njia ambazo zikishindikana basi matumizi sahihi na kila mara ya kondomu ndiyo inakuwa njia pekee ambayo inaweza kunmsaidia mtu kutopata maambukizi ya VVU.

“Kondomu zimekuwa zikitumika hapa nchini kwa muda mrefu sasa, awali zilikuwa zikitumika kama njia ya kupanga uzazi, baada ya kugundulika kwa VVU, tafiti zilifanyika kitaifa na kimatifa na kama ilivyothibitishwa na WHO na UNAIDS ni kwamba kondomu zikitumiwa vizuri zina uwezo mkubwa wa kuzuia maambukizi ya VVU na magonjwa ya zinaa,” alisema Dk. Fatma.

Awali akizungumza wakati wa kumkaribisha mgeni rasmi,Mkurugenzi Mtendaji wa PSI TANZANIA, Daniel Crapper alisema walifikia uamuzi wa kubadilisha mwonekano wa kondomuza Salama Stud ikiwa ni kuitikia wito wa watumiaji wake ambao utafiti uliofanywa ulionesha kuwa wengi walitaka kuhakikishiwa juu ya ubora na uimara wa kondomu zinazozambazwa na PSI.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...