Katibu mkuu wa CHADEMA Dkt.Wilbroad Slaa akimkaribisha katika chama Mwenyekiti wa CHADEMA mkoa wa Mbeya Bw.Sambwee Shitambala ambaye awali alijiuzuru kutokana na tuhuma zilizoelekezwa kwake, Dr.Slaa alimtaka Bw.Shitambala kufanya kazi za chama kwa ushirikiano na kwamba tuhuma zilizoelekezwa kwake zilikuwa ni na uzushi na majungu.
Picha na mdau Rashidi Mkwinda

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 8 mpaka sasa

  1. watu walisha tafuna mpunga longtime !!LOL
    mdau paris

    ReplyDelete
  2. Kama tuhuma zilikuwa za majungu na uzushi, kwa nini Mh Dr Slaa alimtuhumu Bw Shitambala hadharani kabla ya kumpa nafasi ya kujieleza??? Uongozi wa jazba si kitu cha busara.

    ReplyDelete
  3. Mhhh, kwanza unamchafulia mtu jina lake halafu ndo unamwambia sorry. Niliposoma sheria nilijifunza kuwa "innocent until proven guilty" NA SIYO "guilty until proven innocent".

    ReplyDelete
  4. HALAFU JAMAA ANAMWANGALIA KWA HASIRAAAA HUYOOO!!

    ReplyDelete
  5. CHADEMA wameshaanza kuharibu. Sasa wana gogoro kibao. Kila siku tunasikia mapya.

    ReplyDelete
  6. MAJAZBA NAMNA HII MSIPOANGALIA, MPAKA 2015, MTAKUWA HOI. HAPO BADO RUZUKU HAJAPEWA, IKIINGIA, MAFARAKANO. ANGALIENIENI SANA, VINGINEVYO, DR. SLAA KAMWULIZE MREMA, ATAKUAMBIA KILICHOMRUDISHA VUNJO KUGOMBEA UBUNGE.

    INATAKIWA BUSARA SANA SASA HIVI. WATAWACHONGANISHA MPAKA MTASAMBARATIKA. KAMA MNABISHA, SIKU MOJA MTANITAFUTA KUKUBALI MANENO YANGU.

    SIMAMA JIPANGE SAWA SAWA.

    ReplyDelete
  7. "tuhuma zilizoelekezwa kwake zilikuwa ni na uzushi na majungu."

    wanasiasa bwana kwa mujibu wa Shitambala tuhuma zilitokea makao makuu na kumlazimisha ajiuzulu sasa inakuwa uzushi na majungu? sasa makao makuu kwanini wamchafue kisha sasa hivi wajifanye wanamsafisha?
    Siasa ni mchezo mchafu sana

    ReplyDelete
  8. chadema imeanza kunukia udikteka tangu mzee nanihii akuzwe. tunaitaka chadema yetu ya kidemokrasia kama ile vision iliyokusudiwa na kina mzee edwin mtei, bob makani na mh Mbowe. martin.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...