Katika kipindi cha hivi karibuni pamekuwepo migomo ya wanafunzi katika baadhi ya vyuo vya elimu ya juu inayotokana na madai mbalimbali. Katika hali isiyo ya kawaida migomo yote hiyo imekuwa ikihusishwa moja kwa moja na Bodi, kitu ambacho siyo sahihi hata kidogo.

Matukio hayo yanahusisha wanafunzi wa vyuo vinane vilivyotajwa hapa chini. Wanafunzi wa vyuo vyote vilivyotajwa hawana sababu za msingi za kuinyooshea Bodi kidole kwa kuwa matatizo yao ni kati yao na vyuo wanakosoma, kama ilivyoelezwa hapa chini.

Bodi inachukua nafasi hii kutoa taarifa ya msisitizo ili wanafunzi hao na vyuo husika na Umma kwa ujumla waelewe hali halisi ya matukio yaliyojitokeza, tukianzia na Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu Mkwawa (MUCE) ambacho mmoja wa Viongozi wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) wamekitoa kama mfano wakati akitoa tamko la kukurupuka hivi karibuni dhidi ya Bodi, hata bila ya kufanya uchunguzi wa sababu za ndani za migomo ya wanafunzi vyuoni.

Pata tamko zima toka Bodi ya Mikopo

BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...