Habari iliyoifikia Globu ya Jamii usiku huu,inaripoti kwamba Mwanamuziki aliekuwa mpiga Bass wa DDC Mlimani Park Orchestra,Mustafa Ngosha (pichani) ambaye alijulikana zaidi kwa jina maarufu la Ngosha amefariki dunia leo baada ya kusumbuliwa na maradhi kwa muda kidogo.

Ngosha alijiunga na DDC Mlimani Park miaka ya mwanzoni ya 90, akiwa anajulikana kama Charles John Ngosha ila baadae alibadili dini na Kuwa muislam na kupewa jina la Mustafa. Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Amana,Ilala jijini Dar.

Msiba upo nyumbani kwa marehemu Tandale kwa Popobawa jijini Dar es salaam. Kwa mujibu wa mmoja wa wanakamati ya mazishi na mwanamuziki mkongwe Hassan Rehani Bitchuka, mazishi yatafanyika leo saa saba mchana. Ngosha, aliyezaliwa mwaka 1965, ameacha mke na watoto 10

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. M.Ngosha (RIP)Sikinde imepoteza msanii mkubwa...
    /Mdau Vumbi Dekula Sweden

    ReplyDelete
  2. Kalale pahali pema peponi Ngosha,
    wewe ndiye uliyekuwa"Ngouma Lokito"
    wetu tanzania,utakumbukwa na kuheshimiwa daima kwa upigaji wako mahiri wa bass.Pia shukrani zangu kwa wanamuziki wenzetu wote mlioko nyumbani Tanzania kwa kuwa na moyo wa upendo hasa wakati wa misiba ya wanamuziki wenzetu sisi tulioko nje
    ya nchi hufarijika sana tunapowaona mkishiriki ktk.misiba hasa kupitia mitandao mbali mbali,Nawapa pia pole kaka zangu wa Sikinde."Respect"
    Abbu Omar,Prof.Jnr(mwanamuziki)Tokyo,Japan.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...