
Asasi ya Happy Roots, ni asasi ambayo tumekuwa tukifanya nayo kazi kwa muda mrefu sasa, Happy Roots inafanya kazi kitaifa na ina tawi lake Geita mkoani Mwanza na makao makuu yake yapo Mbezi Beach wilaya ya Kinondoni hapa Dar es salaam.
Happy Roots wanafanya kazi kwa kuzunguka maeneo mbalimbali hasa mashuleni ili kuelimisha jamii juu ya athari za dawa za kulevya, kwa kuwa huwa wanazunguka sehemu mbalimbali, katika viwanja vya michezo na kwa wajumbe wa nyumba kumikumi kwa kutumia vifaa na zana duni kuelimisha jamii, waliomba wawezeshwe TV moja (Samsung 29”), Deki ya DVD (Sumsung) moja Deki VHS (LG) moja pamoja na Generator moja. Ili viweze kuwasaidia katika katika kazi zao. Tume kwa kuona umuhimu imewanunulia vifaa hivyo. Vifaa hivyo vina thamani ya Tsh. 2,796,600/=.
Natumaini vifaa hivyo vitawasaidia katika kutimiza majukumu yenu ya kila siku.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...