Timu ya Bongo Fleva ikiwa na kikombe chao mara baada ya kukabidhiwa jioni hii.
Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Silaa akikabidhi kombe kwa nahodha wa timu ya Bongo Fleva, Kharid Ramadhan ‘Tundaman’ baada ya mchezo wa maalumu wa kuchangia waathirika wa milipiko wa mabomu ya Gongo la Mboto. Mchezo huo umefanyika kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam, jioni hii. Bongo Fleva imeshinda 2-0.
Mshambuliaji wa timu ya Bongo Freva,Ali Kiba akijaribu kutaka kumtoka beki wa timu ya Bongo Movie katika mtanange wa Kuchangia maafa ya Gongo La Mboto uliomalizika jioni hii katika uwanja wa Taifa jijini Dar.Bongo Freva iliibuka kidedea kwa mabao 2-0 yaliyotiwa kimyani na mshambuliaji H. Baba katika kipindi cha kwanza cha mchezo.
Kiungo wa Bongo Movie,Ben Kinyaiya akipiga penati na kukosa kwa kupiga nje.
Mshambuliaji wa kushoto wa timu ya Bongo Freva,KR Mullah akimtoka mchezaji wa timu ya Bongo Movie katika mchezo uliopigwa jioni hii katika uwanja wa Taifa.

kwa picha zaidi

BOFYA HAPA.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Ile kesi ya meya wa moshi kumzabua mgambo kwa kufanya kazi yake iko hatua gani vile?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...