Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Mohamed Gharib Bilal, akimfariji Mkurugenzi wa Baraza la Manispaa Zanzibar Rashid Ali Juma (45) alipomtembelea leo katika Hospitali ya Aga khan jijini Dar es salaam alikolazwa kwa matibabu kutokana na kuumia vibaya sehemu za usoni, tumboni, kifuani na ubavuni baada ya kumwagiwa Tindikali na Mtu asiyejulikana, wakati alipokuwa amekaa nje ya Msikiti wa Amani mjini Zanzibar baada ya kumalizika kwa Ibada ya Sala ya Insha saa 2:45 usuku, siku ya Alkhamis . Kwa muujibu wa madaktari wanaomhudumia Mkurugenzi huyo, wamemuambia Makamu wa Rais kuwa hali yake inaendelea Vizuri.

Picha na mdau Amour Nassor wa VPO.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. MMM jamani hawa binadamu wengine kisa kidog mwenzako anakuwazia mabaya kweli jamani mwema wako na mbaya wako uwezi mtambua.

    ReplyDelete
  2. POLE SANA!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...