Mwongoza Watalii Hifadhi ya Taifa ya Mikumi, akitoa maelekezo kuhusiana na Bwawa la Viboko kwa washiriki wa Miss Utalii Tanzania
Kaimu Mhifadhi wa Hifadhi ya Taifa ya ya Mikumi, Apaikunda Mungure, akitoa Maelekezo kwa washiriki Tanapa Miss Utalii Tanzania

Washiriki Miss Utalii Tz, 2011 , Wakipanga Matofali ili kuweka Mazingira ya Hospitali ya Wilaya ya Bagamoyo katika hali ya Usafi
Mtalii Kutoka Hispania, Cosudaren joranky, akitoa Maelezo kwa Washiriki Miss Utalii Tanzania 2011, Katika Bwawa la Viboko kwenye hifadhi ya Mikumi
Baadhi ya Washiriki wa Tanapa Miss Utalii Tanzania 2011, baada ya kuwasili katika Hifadhi ya Taifa ya Mikumi, huku Tembo akipicha chabo nyuma yao
Washiriki Miss Utalii Tanzania, wakiwa katika Mbuyu ulioishi zaidi ya Miaka 500 katika Hifadhi ya Taifa ya Mikumi

Warembo hao leo wamefanya Ziara ya Kihistoria katika Hifadhi ya Mikumi ambapo walifika katika Vivutio mbalimbali vya Utalii vilivyopo katika hifadhi hiyo ikiwemo, mabwawa ya Viboko yaliyosheheni Viboko wakubwa wanaofiki ukubwa wa zaidi ya Nusu tani, wakiwa sambamba na Mamba wakubwa wenye nguvu na urefu wa zaidi ya mita 10.

pia warembo walijionea makundi makubwa ya tembo, Twiga, Nyati, Pundamilia, Swala, Pofu, Mbwa Mwitu, na zaidi ya aina mia nne za ndege wakubwa kwa wadogo.

katika ziara hiyo warembo walipokewa na kaimu mhifadhi wa Mikumi National park Apaikunda Mungure ambaye alielezea kufurahishwa na ujio wa warembo hao ambao alisema kuwa watasaidia sana kutangaza hifadhi hiyo ya taifa.

katika ziara hiyo Miss Utalii Kagera Daissy Mushumbusi mwenye Digrii ya kwanza ya utalii kutoka chuo kikuu cha Moi alinyakua Tuzo ya kuwa barozi wa utalii wa hifadhi ya Taifa ya Mikumi na kuwabwaga warembo wengine 47 wanaoshiriki shindano hilo.

Leo warembo wanaendelea na ziara katika hifadhi ya taifa ya Udzungwa.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. Naona wanachukua notes. Ingefaa kila moja aaandike insha kuhusu walichooana. Ingesaidia katika selection process.

    ReplyDelete
  2. Hapo akiibuka mnyama mkali inakuwaje? Shule inaendelea ama vipi?

    (US Blogger)

    ReplyDelete
  3. Dah kweli nimefurahishwa na hawa mamiss, eti wanavaa gloves za hospitali kwenye kazi ya zege...kwani hawajui kuna gloves za zege na hizo walizovaa?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...