NA VERONICA KAZIMOTO – MAELEZO
Waziri wa Maliasili na Utalii Ezekiel Maige amesema Wizara yake inatarajia kufukua Nyayo za Binadamu wa kale maarufu kama Zamadamu zinazopatikana katika eneo la Laetoli mkoani Arusha ifikapo tarehe 7 Februari, mwaka huu.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Waziri huyo amesema kuwa ufukuaji wa nyayo hizo utafanyika kwa muda wa wiki mbili ambapo takribani milioni mia mbili zinatarajiwa kutumika katika ufukuaji huo.
“Zoezi hili la ufukuaji wa nyayo za Zamadamu litagharimu fedha za kitanzania milioni mia mbili ambazo mpaka sasa zimekwisha anza kutumika na tayari baadhi ya wafanyakazi wameshatanguli katika eneo husika.” Amefafanua Maige.
Waziri Maige amesisitiza kuwa Kukamilika kwa shughuli hii ya ufukuaji kutakuwa mwanzo mzuri wa maandalizi ya kufukua nyayo zote hapo baadaye ambazo zitatafutiwa mazingira mazuri ya kuhifadhi nyayo hizo bila kuharibika.
Nyayo za zamadamu wenye umri wa miaka milioni 3.6 zilivumbuliwa na mtafiti maarufu Dkt mary Leakey mwaka 1978 katika eneo la Engarusi huko Laetoli ndani ya hifadhi ya Ngorongoro na nyayo hizo zimehifadhiwa kwenye mwamba wa Volcano.
Nyao hizo zilizotunzwa kwenye mwamba wa Volcano sio tu kwamba zinatunza kumbukumbu za aina ya wanyama na ndege walioishi wakati huo bali pia ni kielezo muhimu kinachoonesha kuwa kwa kipindi hicho binadamu alikuwa anasimama na kutembea kwa miguu miwili.
Waziri wa Maliasili na Utalii Ezekiel Maige amesema Wizara yake inatarajia kufukua Nyayo za Binadamu wa kale maarufu kama Zamadamu zinazopatikana katika eneo la Laetoli mkoani Arusha ifikapo tarehe 7 Februari, mwaka huu.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Waziri huyo amesema kuwa ufukuaji wa nyayo hizo utafanyika kwa muda wa wiki mbili ambapo takribani milioni mia mbili zinatarajiwa kutumika katika ufukuaji huo.
“Zoezi hili la ufukuaji wa nyayo za Zamadamu litagharimu fedha za kitanzania milioni mia mbili ambazo mpaka sasa zimekwisha anza kutumika na tayari baadhi ya wafanyakazi wameshatanguli katika eneo husika.” Amefafanua Maige.
Waziri Maige amesisitiza kuwa Kukamilika kwa shughuli hii ya ufukuaji kutakuwa mwanzo mzuri wa maandalizi ya kufukua nyayo zote hapo baadaye ambazo zitatafutiwa mazingira mazuri ya kuhifadhi nyayo hizo bila kuharibika.
Nyayo za zamadamu wenye umri wa miaka milioni 3.6 zilivumbuliwa na mtafiti maarufu Dkt mary Leakey mwaka 1978 katika eneo la Engarusi huko Laetoli ndani ya hifadhi ya Ngorongoro na nyayo hizo zimehifadhiwa kwenye mwamba wa Volcano.
Nyao hizo zilizotunzwa kwenye mwamba wa Volcano sio tu kwamba zinatunza kumbukumbu za aina ya wanyama na ndege walioishi wakati huo bali pia ni kielezo muhimu kinachoonesha kuwa kwa kipindi hicho binadamu alikuwa anasimama na kutembea kwa miguu miwili.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...