Mwaandaaji wa Onyesho la Lady in Red 2011,Asia Idarous akifafanua jambo mbele ya waandishi wa habari (hawapo pichani) mapema leo asubuhi,jijini Dar kuhusiana na mchakato mzima wa onyesho hilo lenye kila aina ya msisimko lifanyikapo.
Pichani kati ni Meneja kinywaji cha Redds ambao ndio wadhamini wakuu wa onyesho la Lady in Redds (TBL),Kabula Nshimo akifafanua zaidi mbele ya waandishi wa habari kuhusiana na onyesho hilo,ndani ya moja ya ukumbi wa hoteli ya Regency,Mikocheni jijini Dar.kushoto ni Mwaandaaji wa Onyesho hilo la Lady in Red 2011,Asia Idarous kutoka Fabak Fashions na kulia ni Diana Ibrahimu kutoka Beatiful Agency.

Onyesho hilo limepangwa kufanyika februari 11,ndani ya hoteli ya Moven pick,ambapo kiingilio kimepangwa kuwa ni sh 20,000/=kwa kila kichwa.Aidha katika onyesho hilo wabunifu mahiri wa mavazi 20 wataonyesha mitindo ya Kitanzania,kwa kuwataja wachache atakuwepo Ally Rhemtullah,Mustafa Hassanal,Manju Msita,Khadija Mwanamboka,Fransisca Shirima,Zamda George,Dayana Magesa,Kemi Kalikawe,Martin Kadinda,Joiyce na wengineo kibao.

Katika onyesho hilo pia kutakuwepo na burudani mbalimbali itakayotolewa,litakuwepo kundi la Babloom taarab,Trio Band,Baby Madaha,kikundi cha ngoma za asili Simba Traditional Dance pamoja na msanii mahiri wa kizazi kipya Chid Benz.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...