Pamoja na mambo mengine, Balozi wetu Marekani Mh Mwanaidi Maajar aliwasifu Watanzania wa Washington DC Metro kwa kuunda kamati ya muda itayopelekea kuundwa kwa jumuiya rasmi itayounganisha wadau wote. Pia alitoa nafasi ya watanzania hao kuweza kwenda kumwona ofisini kwake kila Jumanne na kufanikisha uchaguzi wa kamati ya katiba ya jumuiya ya watanzania.
Aidha mh. Balozi aliwataka maafisa wake wa ubalozi kujitambulisha kwa Watanzania wenzao na pia kutoa mawasiliano yao wazi ikiwemo simu na barua pepe na kuweka bayana kuwa milango ya mawasiliano kati ya ubalozi na watanzania iko wazi.
Balozi pia alikuwa wa kwanza kutoa mawasiliano yake wazi mbele ya watanzania wa Washington Dc ikiwemo mpaka nambari yake ya mkononi kitu ambacho hakijawahi kuonekana.
Kwa picha zaidi za Washington DC
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...