Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala,Mh. Jerry Slaa akiwa ndani ya gari aina ya Iveco Euro Cargo ikiwa ni moja kati ya magari matatu ya kubebea taka ngumu pamoja na vifaa maalum vya kuhifadhia taka hizo vilivyonunuliwa na Halmashauri ya Manispaa ya Ilala kwa ajili ya kukidhi mahitaji ya wananchi wake,shughuli hii imefanyika mapema leo asubuhi ndani ya yadi ya kampuni ya INCAR Tanzania iliyopo Pugu Road.Magari hayo pamoja na Vifaa hivyo vya kuhifadhia taka vimegharimu kiasi cha shilingi mil. 800.
Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala,Mh. Jerry Slaa akiwa katika mazungumzo na Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya INCAR Tanzania,Bw. Rajeev Puri.
Magari Mawili kati ya Matatu yaliyinunuliwa na Halmashauri ya Manispaa ya Ilala kwa ajili ya kubebea taka ngumu kwa wakazi wa Manispaa hiyo.
Mh. Jerry Slaa akiwa pamoja na viongozi wengine wa Manispaa ya Ilala wakiangalia vifaa maalum ya kuhifadhia taka ngumu vilivyonunuliwa na Halmashauri ya Manispaa ya Ilala asubuhi ya leo.
Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala,Mh. Jerry Slaa (kulia) akiwa katika picha ya pamoja na maafisa wa Halmashauri ya Ilala pamoja na wafanyakazi wa Kampuni ya INCAR Tanzania mapema leo asubuhi wakati walipokwenda kuchukua magari hayo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. sawa mambo mswanu lakini tutakuja kuambiwa kuwa yalikuwa na hujuma au yalinunuliwa machakavu kama yalivyokuwa ya wilaya ya kinondoni yetu macho kemcho taka pesa gapi pitisha veve kwa macho tu tunaona

    ReplyDelete
  2. duh huyu meya naona kweli ni damu changa inafanya kazi. Naamini iko siku dar itabadilika kama tutapata watu kama hawa. huu ni mwanzo tu naamini.

    ReplyDelete
  3. haya ndo mambo sasa. hayo magari yamegarimu milioni 800 ikiwa na maana kila gari na kifaa chake ni Tsh. Milioni 267. Gaharama hii ni ya chini kuliko mashangiungi ya Serikali (kama lile alilolipiga chenga Mh. Pinda).

    Tukiacha kununua kila shangingi tuna gari moja na vifaa vya kuhifadhia taka. Maendeleo yataletwa ikiwa tu Serikali itaamua kuchagua....kupanga ni kuchangua.(JK Nyerere),

    BIG UP kwa ILALA MUNICIPAL

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...