Home
Unlabelled
hotuba ya JK ya mwisho wa mwezi wa februari 2011
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Most read Swahili blog on earth
Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.
Nadhani suluhisho hapa ni kwa viongozi wote wakuu wa vyama ikiwemo CCM kukaa pamoja na kujadiliana wakati wa matatizo ya dharura. Nadhani kama wenyeviti na makatibu wakuu wa vyama (CCM na wapinzani) wakikutana wanaweza wakatoka na mawazo yenye kujenga. Tuache siasa wakati wa matatizo serious kama ukosefu wa umeme na chakula.
ReplyDeletePia sidhani kama viongozi wa CCM akiwemo Rais wanatakiwa kuongelea maswala ya machafuko na umwagaji damu. Hii inasabisha hayo mawazo kuingia akilini mwa watu. Sidhani kama kuna mtu anamawazo ya kumwaga damu. Wanachofanya CHADEMA ni siasa tu na sidhani kama kuna haja ya CCM kuogopa. Wao kama kweli wanadhamira ya kuondoa matatizo ya wananchi wawashirikishe pia viongozi wa upinzani hasa wakati wa dharura na kupata mawazo. Viongozi wakuu wa vyama waache viburi vyao, wakae pamoja. Hakuna aliyemjuaji kuliko mwenzie na hakuna mtu anayeweza kupredict future with certainty hasa ikiwa unategemea mvua kwa kiasi kikubwa katika maisha yako ikiwemo mvua kwenye umeme, mvua kwenye chakula, etc....
hotuba ya Raisi ni ya muhimu na imejieleza kimsingi.Ina udadisi wa muhimu.Lakini Tanzania ni nchi ya amani na tunapenda amani yetu.Lakini viongozi inabidi wajue kwamba sio inchi ya wapumbavu wapendao amani.Subura yavuta heri,hilo linajulikana lakini kuna mambo mengi watanzania wana maswali?utaratibu wa kujibu maswali na kufatilia malalamiko ni mbovu sana na hamna mfumo wa wazi wa kuweza kifatilia jambo.
ReplyDeleteSiungi mkono maandamano ya vurugu lakini lazima viongozi walio madarakani wajue kwamba watanzania tutachoka na wakiendelea kubweteka mambo hayatakwenda sambamba.
Lazima ieleweke kwamba tunahitaji usawa kati ya watu.Kupunguza rushwa,kupunguza mgawanyiko kati ya matajiri na maskini.Mtu hawezi kushindwa kula na kuishi na amani na mtu mwenye gari la mamilioni kwa amani.Ndio kila Mbuzi hula kwa urefu wa kamba yake lakini kwamba yangu ikiwa fupi nitakula kamba ikatike na ninakuja kula kwako.Nawaonya wanaojilimbikizia mali bila kujali maslai ya watanzania wengine.Tanzania ni yetu sote na lazima tumjali kila mwananchi