CCM Manchester inapenda kutoa shukrani zao za dhati kwa wanachama wote na wanajumuiya wa Manchester na vitongoji vyake pamoja na uongozi wa CCM UK, Jumuiya ya Watanzania UK, Wananchama wote wa CCM miji mbalimbali, Watanzania wote UK bila kusahau jumuiya ya Wasomali Manchester kwa kushiriki kwa hali na mali kuweza fanikisha mazishi ya kada wetu wa CCM, kaka yetu, ndugu yetu Modibo Keita alietangulia mbele ya haki.

Tunawashukuru sana kwa kujitokeza kwenu na kuweza kufanikisha swala zima la mazishi ya ndugu yetu huyo.

Mungu amlaze mahali pema peponi ndugu yetu Modibo Keita.

Amin.

Uongozi CCM Manchester

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Ingependeza kama ungeshukuru wale wote waliofanikisha mazishi ya ndugu Keita, sisi wengine hatuna itikadi za KiCCM ila tulikuwepo

    Mdau Manchester

    ReplyDelete
  2. Umoja na Upendo ulio onyeshwa Manchester wakati wa mazishi ya aliyekua mpiganaji wa maendeleo ya jumuiya yetu kama Watanzania, ni wa kupongezwa na kuigwa.
    Wazee,vijana,watoto waume kwa wake toka Manchester na mikoa mbalimbali ya UK hamkusita kuacha kazi na majukumu yenu ili kushiriki kumpa heshima na hifadhi ya mwisho ndugu yetu Keita Denis:HONGERA SANA.

    MUNGU AWABARIKI.

    MAINA ANG'IELA OWINO
    UK

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...