Mamlaka ya viwanja vya ndege Tanzania yatoa msaada kwa wahanga wa mabomu gongo la mboto,misaada hiyo ni pamoja na mchele, maharage,unga,sukari na taulo za kike.

akikabidhi misaada hiyo kwa niaba ya uongozi na wafanyakazi wa mamlaka ya viwanja vya ndege,meneja mariasili watu alisema " tumeguswa sana na maafa hayo yaliyowatokea wananchi wa gongo la mboto ukizingatia ni majirani zetu, kama taasisi tunawajibu wa kuwasaidia kwa hali na mali waaathirika wa mlipuko huo wa mabomu".

kutokana na kuwa jirani na eneo la mlipuko mamlaka ya viwanja vya ndege iliathirika kwa kiasi flani na mlipuko huo ikiwemo ku cancel safari za ndege kwa muda ili kuhakikisha usalama wa kiwanja.

kaimu Mkuu wa mkoa akipokea misaada hiyo, aliushukuru uongozi huo kwa misaada na kuweza kuwakumbuka hata kinamama maana wao ni katika kundi lililoathirika zaidi na mlipuko huo kutokana na kuunguliwa na kila kitu zikiwemo nguo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Wahanga?! teh teh teh, Michuzi si ulikuwepo kwenye semina iliyoendeshwa na Dk. Harrison Mwakyembe?! Kazi kweli kweli!

    ReplyDelete
  2. wahanga wanapaje misaada kama walijilipua?? huwezi toa msaada kwa mtu ambaye hayupo. Hawa ni WAATHIRIKA wa mabomu ya Gongo la Mboto.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...