MWALIKO WA WADAU KUTOA MAONI MBELE YA KAMATI YA BUNGE YA KATIBA SHERIA NA UTAWALA BORA KUHUSU MUSWADA WA SHERIA YA MABADILIKO YA KATIBA YA NCHI (THE CONSTITUTIONAL REVIEW BILL, 2011)
Kwa mujibu wa Kanuni ya 114(9) ya kanuni za kudumu za Bunge, kamati ya Bunge ya Katiba, sheria na Utawala Bora inawaalika wananchi na wadau wote kushiriki katika mkutano wa kupokea maoni kuhusu Muswada wa Sheria ya Mabadiliko ya katiba ili kupata maoni na ushauri wao kwa ajili ya kuboresha Muswada huo. Mikutano ya kupokea maoni hayo itafanyika tarehe 7, 8 na ikibidi tarehe 9 April, 2011 Mjini Dar es salaam na Dodoma kama jedwali hapa chini linavyoonyesha:
*7 – 8/April/2011 Itakuwa Dar es salaam
ukumbi wa Karimjee Saa 3 Asubuhi
*7 – 8/April/2011 Itakuwa Dodoma
Ukumbi wa Msekwa.
Kwa taarifa hii, wananchi wote kwa ujumla wanaalikwa kushiriki kwenye mikutano hii kwa ajili ya kutoa maoni yao kama inavyoonekana katika jedwali hapo juu.
Imetolewa na:
Ofisi ya Bunge Idara ya Habari, Elimu kwa
Umma na Uhusiano wa Kimataifa
Dar es Salaam
5 Aprili 2011
Katiba ya nchi ni suala kubwa sana kwani linatugusa sisi sote. Serikali imekuwa ikipigiwa kelele za katiba mpya tokea 1992, Kinachonishangaza hapa badala ya wao kuandaa mchakato from the drawing board wameng'ang'ania maboresho maboresho, halafu ni nini hasa kinachowafanya watumie zima moto kwenye suala hili?, kwa nini wasitoe muda wa kutosha kwa wadau kutoa mawazo yao kuhusu nini kifanyike, kama ni maboresho au kuandika upya na iandikwe vipi?. Kwa nini wanataka kuburuza wananchi kwa jambo ambalo tukiwa makini linaweza fanyika once and for all? kuliko hizi half cooked measures za kudanganyia watoto peremende.
ReplyDeleteMichuzi natumai hutabania hii comment
Kuna namna yo yote inayotuwezesha na sisi wa ughaibuni kushiriki kwa kutoa maoni yetu?
ReplyDeleteNa siye wa ughaibuni tuwezeshe hii. Na hiyo ya zamani ipo kwenye link gani ili tukiisoma tujue nini ni outdated. Sheria twaziona tu mitaani lakini wapi zimeandikwa hatuzijui....
ReplyDeleteTupeni link
This is a very short notice. Hii ni jambo nyeti sana. Mngetupa taarifa muda mrefu...
ReplyDelete