Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dk. Jakaya Mrisho Kikwete akiwatambulisha kwa Wanachama wa Chama cha Mapinduzi Mkoa Dodoma aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema Mkoa wa Mbeya Sambweli Shtambala kulia na aliyekuwa Katibu Muenezi wa Chama hicho Wilaya ya Ileje Heri Kayuni baada ya kukihama chama hicho na kujiunga na Chama cha Mapinduzi CCM kwenye hafla iliyofanyika katika Viwanja vya Makao Makuu ya CCM Mjini Dodoma leo.
Aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema Mkoa wa Mbeya Sambweli Shtambala na Katibu Muenezi wa Chama Hicho Wilaya ya Ileje Heri Kayuni, wakila kiapo cha Utii na kuwa waaminifu kukilinda na kukitetea Chama cha Mapinduzi CCM baada ya kujiunga na Chama cha Mapinduzi CCM na kukabidhi wa Kadi za Chama Cha Mapinduzi CCM na Mwenyekiti wa CCM Taifa Rais Jakaya Mrisho Kikwete katika hafla iliyofanyika kwenye Viwanja vya Makao Makuu ya CCM Mjini Dodoma leo. Amour Nassor VPO.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 6 mpaka sasa

  1. Hongereni kwa maamuzi yenu ya busara. Ila tunataka CCM ijivue gamba ili iturejeshee imani tuliyokuwa nayo tangu mwanzo. Japo juhudi tunaziona lakini bado ni kasi ndogo bado. JK kaza buti unaanza kujivua gamba

    ReplyDelete
  2. hawa viongozi wanaohama kutoka chama kimoja kwenda kingine, sijui watatueleza nn tuwaelewe. Mana kwa macho ya kawaida tunajua ni maslahi tu ndo yanayowafanya wasitulie. They have decided to invest in politics na hiyo ndio njia pekee ya wao kuishi. Hakuna jipya. Watahama sana. Ccm itabaki kuwa ccm na chadema the same way. Wananchi wanaangalia hali yao ya kimaisha na sio kuangalia nani kahama kwenda wapi. Haitusaidii.

    ReplyDelete
  3. Njaa tu hizi hakuna lolote la kusema wamependa sera za chama tawala nina uhakika hata ukiwauliza kuwa ilani ya chama tawala inasema nini kuhusu elimu watakuwa hawajui. CCM sasa hivi haina sera ya kuwapa ulaji watu wanaohamia kutoka vyama vingine kwa hiyo kama motive yao ilikuwa something then wajue ni patupu.

    ReplyDelete
  4. CHADEMA halitushangazi sana hilo. Sambweli Shitambala siku nyingi alikuwa ameisaliti chadema Ni mtu hakutulia hasa baada ya kukosa ubunge. CCM itawanunua wengi tu maana inakaribia kufa.

    ReplyDelete
  5. Hata walivyokua chadema walikula kiapo hivi hivi na sasa wanakikana, hili jina la "Kiapo" wangelibadilisha kwa wanasiasa maana wanakufuru, utasikia akisema "Nikiwa na akili zangu timamu, naapa kuilinda na kuitetea sijui nini nini..". Sasa kuna mawili, either wakati wa kuapa alikua hana akili timamu kama alivyosema, au wakati wa kuhama anakua hana akili fresh, au vyote before and after.

    ReplyDelete
  6. Na Prof. Safari mnemwonaje. Chadema ni ya kabila na dini fulani, watu wameshangamua. Kalagabaho.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...