ULE usemi “usitathmini kitabu kwa kuangalia jalada lake ” una maana kubwa unapomzungumzia Susan Mashibe, mhandisi wa masuala ya ndege na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni mbili zinazoshughulika na masuala ya anga, lakini unapokutana naye kwa mara ya kwanza huwezi kuamini kama mwanadada huyo ana sifa hizo ndio maana nikakumbuka ule usemi, ‘usitathmini kitabu kwa kuangalia jalada lake.’ Kuthibitisha uwezo wake mkubwa katika fani hiyo, hivi karibuni Mashibe alichaguliwa na Taasisi ya World Economic Forum (WEF) kuingia katika kundi dogo la heshima la vijana waliothibitisha vipaji vya uongozi la Viongozi Vijana Duniani (Young Global Leader- YGL)) kwa mwaka huu wa 2011. Sambamba na Susan, Mtanzania mwingine Elsie Kanza, Mshauri wa Uchumi wa Rais Jakaya Mrisho Kikwete amechaguliwa na taasisi hiyo pia kuingia katika kundi hilo. Mashibe na Kanza walichaguliwa kutoka miongoni mwa viongozi vijana 5,000 waliopendekezwa kutoka duniani pote na hatimaye kupitishwa katika mchujo na kuchaguliwa kwenye mchujo mkali na Kamati Maalumu chini ya uenyekiti wa Malkia Rania Al Abdullah wa Ufalme wa Hashemite wa Jordan. Nenda Habari leo upate stori nzima ya mwanadada Susan Mashibe
Home
Unlabelled
wanawake wakiwezeshwa wanaweza: Kutana na Suzan Mashibe, mmiliki wa kampuni inayoshughulikia ndege binfsi maarufu kama executive jets
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...