Rais Jakaya Kikwete akiaga baada ya kuhani msiba wa Marehemu Athumani Hassan
Mwinyimvua mtaa wa Matombo Magomeni Mwembechai jijini Dar leo

Rais Jakaya Kikwete akihani msiba wa Marehemu Athumani Hassan Mwinyimvua leo

 Rais Jakaya Kikwete na Mama Salma Kikwete wakimfarihi Mama Mwajuma Mwinyhimvua, mjane wa Marehemu Athumani Hassan Mwinyimvua leo
 Rais Jakaya Kikwete akisalimiana na watoto baada ya kuhani msiba wa Marehemu Mwinyimvua
 Rais Jakaya Kikwete akisalimiana na wanafamilia wa Marehemu Sheikh Yahya Hussein baada ya kuhani msiba wa mnajimu huyo maarufu leo nyumbani kwa marehemu Mwembechai
 Hassan Yahaya Hussein, mtoto mkubwa wa Marehemu Sheikh Yahaya Hussein, akimkaribisha Rais Kikwete na Mama Salma Kikwete walioenda kuhani msiba leo
Rais Kikwete na Mama Salma Kikwete wakimfariji mjane wa Sheikh Yahya Hussein (aliyejifunika) leo

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 6 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 22, 2011

    JAKAYA KWA MSIBA TU NAMPA BIG UP,INAONYESHA KWELI MTU WA WATU.VIONGOZI WENGINE WAIGE MFANO HUU.

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 22, 2011

    Hata mimi nimetiwa moyo na tabia hii ya JK. kutembelea watu wanaohitaji faraja. Hili ni jambo zuri sana. Nakupa pongezi Mheshimiwa.

    Mchungaji

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 22, 2011

    Jamani huo ujifunikaji wa mfiwa hata kwa rais, au ndio imani hairuhusu kabisa? Makubwa!

    ReplyDelete
  4. AnonymousMay 22, 2011

    we mchangiaji wa tatu ni mbaguzi wa dini. kila mtu ana uhuru wa kuvaa atakavyo.

    ReplyDelete
  5. AnonymousMay 23, 2011

    huo ujifunikaji ni mila na sio imani, maana mwanamke wa kiislam anatakiwa ajihifadhi mwili wake na nywele zake kwa hijabu wakati mumewe akiwa hai na sio kujifunikiliza wakati mtu kafa, unatakiwa upige hijabu yako kisawasawa siku zote, hayo ni mambo ya kizuka ya mila na tamauni.

    ReplyDelete
  6. AnonymousMay 23, 2011

    Mdau hapo juu, hiyo sio mila na tamaduni! Mila na tamaduni za watanzania ni kutembea uchi kabla hazijakuja dini! hiyo ni dini ya kiislamu! umesema vizuri kuwa mwanamke wakati wote anatakiwa ajihifadhi! lakini inapotokea amefiwa na mumewe hiyo hijab inaidi! haruhusiwi mwanamke kuonana na watu ambao wanaweza kumuoa! na hata sauti hatakiwi kuzungumza kubwa ! anatakiwa awe anaomboleza kifo cha mumewe ili apate RADHI ZA ALLAH SWT. na kama alivosema mdau wa juu ambae baadae akachemka ni kwamba mwanamke wakati wote anatakiwa ajifunike full Hijab mwili wake ni kwa ajili ya mumewe tu "FOR HER HUSBAND'S EYES ONLY" Nashangaa kule juu mke wa mwinyimvua yupo waziiiii! kizuka hatakiwi awe hivi! na we mdau wa hapo juu Mwenye Ez Mungu hajui rais wala nini ! watu wote sawa kwa Mungu kwahiyo sio alivokuja rais basi mtu unavunja amri za ALLAH eti kwa kuwa rais wamenifurahisha sana hawa !

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...