Mama Mpendwa,
Ilikuwa saa 4.30 usiku,tarehe 29 Mei 2008 ulipotutoka.Nakumbuka nilipopigiwa simu kufahamishwa kuwa Bwana Amekutwaa,nilidhani ni ndoto tu.Japo ulikuwa umepoteza fahamu kwa zaidi ya miezi mitatu kabla ya kukumbwa na mauti sote tuliamini kuwa siku moja ungeamka ukiwa mzima.Mama,japo leo ni miaka mitatu tangu ututoke,bado nahisi niko ndotoni na nimeshindwa kabisa kukubaliana na ukweli kwamba haupo nasi.Mara kwa mara nakuona ndotoni,lakini napoamka nagundua ni ndoto tu,na hiyo inazidisha uchungu na majonzi.
Baba Mzee Chahali,uliyeishi nae katika ndoa kwa miaka 53,anaendelea kukukumbuka mno.Ni vigumu zaidi kwake kukabiliana na kututoka kwako kwa vile ulikuwa ni rafiki yake mkuu,mtu wake wa karibu kabisa na kila kitu kwake kama ilivyo kwetu.Mapacha, Kulwa (Peter) na Doto (Paul) nao wameendelea kuwa na wakati mgumu kwa vile wewe ulikuwa zaidi ya mama yao.Walikutania,walicheka nawe,walikusaidia kazi za nyumbani,walikwambia furaha na majonzi yao,na waliringa kuwa na mzazi mwenye upendo kama wewe.
Japosiku zote tangu ututoke tumekuwa na wakati mgumu sana,siku hii ya leo tunapoadhimisha miaka mitatu ya kifo chako ni ngumu zaidi kwetu.Inaleta kumbukumbu zisizoelezeka na zisizostahimilika.
Kazi ya Mungu haina makosa.Tukijiuliza sana kwanini alikuchukua wakati bado tunakuhitaji sana tutakuwa tunakufuru.Tunajaribu kujifariji kwa kuamini kuwa alikuchukua kwa vile alikupenda zaidi yetu.Na tunajitahidi pia kujiridhisha kuwa huko ulipo unapata pumziko la amani na unaangaziwa mwanga wa milele ukistarehe kwa amani.Japo haupo nasi kimwili lakini siku zote tupo nawe kiroho.
Pumziko la Milele Akupe Ee Bwana na Mwanga wa Milele Akuangazie Ustarehe Kwa Amani,Amen.
Evarist Chahali
Ilikuwa saa 4.30 usiku,tarehe 29 Mei 2008 ulipotutoka.Nakumbuka nilipopigiwa simu kufahamishwa kuwa Bwana Amekutwaa,nilidhani ni ndoto tu.Japo ulikuwa umepoteza fahamu kwa zaidi ya miezi mitatu kabla ya kukumbwa na mauti sote tuliamini kuwa siku moja ungeamka ukiwa mzima.Mama,japo leo ni miaka mitatu tangu ututoke,bado nahisi niko ndotoni na nimeshindwa kabisa kukubaliana na ukweli kwamba haupo nasi.Mara kwa mara nakuona ndotoni,lakini napoamka nagundua ni ndoto tu,na hiyo inazidisha uchungu na majonzi.
Baba Mzee Chahali,uliyeishi nae katika ndoa kwa miaka 53,anaendelea kukukumbuka mno.Ni vigumu zaidi kwake kukabiliana na kututoka kwako kwa vile ulikuwa ni rafiki yake mkuu,mtu wake wa karibu kabisa na kila kitu kwake kama ilivyo kwetu.Mapacha, Kulwa (Peter) na Doto (Paul) nao wameendelea kuwa na wakati mgumu kwa vile wewe ulikuwa zaidi ya mama yao.Walikutania,walicheka nawe,walikusaidia kazi za nyumbani,walikwambia furaha na majonzi yao,na waliringa kuwa na mzazi mwenye upendo kama wewe.
Japosiku zote tangu ututoke tumekuwa na wakati mgumu sana,siku hii ya leo tunapoadhimisha miaka mitatu ya kifo chako ni ngumu zaidi kwetu.Inaleta kumbukumbu zisizoelezeka na zisizostahimilika.
Kazi ya Mungu haina makosa.Tukijiuliza sana kwanini alikuchukua wakati bado tunakuhitaji sana tutakuwa tunakufuru.Tunajaribu kujifariji kwa kuamini kuwa alikuchukua kwa vile alikupenda zaidi yetu.Na tunajitahidi pia kujiridhisha kuwa huko ulipo unapata pumziko la amani na unaangaziwa mwanga wa milele ukistarehe kwa amani.Japo haupo nasi kimwili lakini siku zote tupo nawe kiroho.
Pumziko la Milele Akupe Ee Bwana na Mwanga wa Milele Akuangazie Ustarehe Kwa Amani,Amen.
Evarist Chahali
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...