Kamishna wa Bima Tanzania Ndugu Israel Kamuzora akiongea na wafanyabiashara ya bima (mameneja na maofisa waandamizi wa makampuni mbalimbali ya bima) mkoani Arusha ambapo alisisitiza umuhimu wa kufanyakazi kwa kufuata sheria,kanuni na taratibu zilizowekwa na nchi. Kamishna alisisitiza zaidi juu ya umuhimi wa kutoa huduma bora kwa wateja wa bima nchini.
Mkuu wa Mamlaka ya usimamizi wa Bima kanda ya Kaskazini Bibi Stella Rutaguza akifungua kikao cha wafanyabiashara wa bima (mameneja na maofisa waandamizi wa makampuni mbalimbali ya bima) mkoani Arusha hivi karibuni.
Wafanyabiashara wa Bima mkoani Arusha pamoja na wafanyakazi wa mamlaka ya Bima kanda ya kaskazini wakiwa kwenye picha ya pamoja mara baada ya kikao chao katika hotel ya Kibopalace.

Mamlaka ya usimamizi wa shughuli za bima nchini imefungua ofisi kanda ya Kaskazini Jijini Arusha. Ofisi hii ya kanda ya kaskazini inajumuisha mikoa ya Kilimanjaro,Tanga,Manyara na Arusha.

Akiongea na wadau wa Bima mkoani Arusha hivi karibuni, Kamishana wa Bima Tanzania Ndugu Israel Kamuzora,alieleza kuwa madhumuni ya kufungua ofisi hii ni kupeleka huduma zinazotolewa na Mamlaka hiyo karibu zaidi na wananchi.

Huduma zinazotolewa na ofisi hii ni kusajili makampuni,madalali na mawakala wa bima Nchini, kusajili wakadiriaji wa hasara wa mali na ajali (Insurance assessors and Loss adjusters), kufanya ukaguzi kwenye makampuni ya bima,kutoa elimu ya bima kwa umma na kusikiliza malalamiko ya wateja wa bima nchini.

kwa picha zaidi
Link
BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...