
Pichani kulia na kushoto (Rolland Barnabas na Francisco Nyambo) wakishangilia ushindi wao wa kuingia kwenye msimu wa dhahabu unaoendelea na serengeti fiesta freestyle 2011,ndani ya Lips Club,Isamilo jijini Mwanza.Washiriki hawa watajiunga na wenzao kutoka mikoa mingine na kutinga ndani ya jiji la Dar kutimiza kile kilele cha msimu wa dhahabu unaoendelea na Serengeti Fiesta 2011,hapo baadaye.

Majaji wakionekana kuduwaa kimtindo mara baada ya ukumbi kulipukwa na mayowe,wakati wa kumtaja mkali wa msimu wa dhahabu unaoendelea na serengeti fiesta freestyle 2011,ndani kiota cha maraha cha Lips Club,Isamilo jijini Mwanza jioni ya leo.

Washabiki kadhaa walijitokeza kuwapngeza wenzao mara baada ya kutajwa kuwa wote wawili,yaani Rolland Barnabas na Francisco Nyambo ndio waliofanikiwa kunyakuwa ushindi mnono wa msimu wa dhahabu unaoendelea na Serengeti Fiesta Freestyle 2011 kati ya washiriki wapato 40.

Ulifika wakati wa kumtangaza mshindi wa msimu wa dhahabu unaoendelea na Serengeti Fiesta freestlye 2011,Pichani shoto ni Mratibu Mkuu wa shindano hilo Fatma Hassan a.k.a Dj Fetty akizungumza jambo kabla ya kumtaja mshindi jioni ya leo ndani ya Lips Club,Isamilo jijini Mwanza,anaefuata ni mshiriki aliyeingia fainali aitwaye Rolland Barnabas,na mwisho kulia ni mshiriki mwingine aliyeingia fainali aitwaye Francisco Nyambo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...