Spika wa Bunge la Muunganoi wa Tanzania Mhe. Anne Makinda akifungua semina ya majadiliano na viongozi wa vyama vya siasa visivyo na wabunge Bungeni kuhusu uanzishwaji wa chombo cha kupokea maoni ya wananchi juu ya uundwaji wa Katiba Mpya ofisini kwake leo 17/05/2011. Huu ni uratibu mpya ambao Ofisi ya Spika imejiwekea kwa lengo la kukutana na kujadiliana na wadau mbalimbali wa kisiasa, Taasisi za dini, sekta binafsi na vyombo vya habari ili kujenga msingi imara wa mjadala mpana wa uundwaji wa Katiba mpya. Leo Spika Makinda amekutana na wadau kutoka vyama vya siasa vilivyosajiliwa vya UMD, AFP,NLD, UPDP, NRA na APPT-Maendeleo. Kushoto kwa Spika ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Katiba na Sheria Mhe. Angela Kairuki
Spika wa Bunge la Muunganoi wa Tanzania Mhe. Anne Makinda akifungua semina ya majadiliano na viongozi wa vyama vya siasa visivyo na wabunge Bungeni kuhusu uanzishwaji wa chombo cha kupokea maoni ya wananchi juu ya uundwaji wa Katiba Mpya ofisini kwake leo 17/05/2011. Huu ni uratibu mpya ambao Ofisi ya Spika imejiwekea kwa lengo la kukutana na kujadiliana na wadau mbalimbali wa kisiasa, Taasisi za dini, sekta binafsi na vyombo vya habari ili kujenga msingi imara wa mjadala mpana wa uundwaji wa Katiba mpya. Leo Spika Makinda amekutana na wadau kutoka vyama vya siasa vilivyosajiliwa vya UMD, AFP,NLD, UPDP, NRA na APPT-Maendeleo. Kushoto kwa Spika ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Katiba na Sheria Mhe. Angela Kairuki





kama ni kuuenzi umoja wa kitaifa basi katiba ishughulikie matatizo ya udini yanayotugawa. Iwepo sheria ya kuchunguza na kuadhibu wabaguzi kwa misingi ya dini makazini, sehemu za huduma kama sibitali, sehemu za sheria kama polisi na mahakamani, mashuleni n.k.
ReplyDeleteTusiache dhamana ya kukemea udini iwe mikononi mwa mabosi ambao wanaweza kuwa wadini na wazalendo wa dini zaidi kuliko taifa.
Dhamana ya kufuta udini iwe mikononi mwa dola kisheria/kikatiba.
Sidhani kwa hilo kama tutachafua amani bali kuikomaza. Tusipofanya hivyo basi mjuwe tunafuga wadini serikalini na sehemu nyengine za umma.
Watu hawapendi kuzungumzia tatizo la udini nalo linaendelea kumea mizizi na kuleta matunda machungu. Tuung'owe huu mti kisheria. Tukifumba macho, leo ni mimi kesho ni mwanao.
ReplyDeleteKukemea tuu kwa kulaani ubaguzi hakutoshi.
Nahisi hutajisikia vyema mwanao akimaliza shule akanyimwa ajira kwa misingi ya kidini au kikabila halafu hana namna wala sehemu ya kulalamika kisheria.
Ndiyo nchi hii inafuata utawala wa kisheria, lazima kila tatizo litatuliwe kisheria, hata ubaguzi.
ReplyDeleteKama inafikia watu kubadilisha majina ili kuepuka ubaguzi basi serikali imelala saana au ni lengo la baadhi ya wakuu serikalini kwa makusudi kisirisiri.
ReplyDeleteKatiba ya sasa inatakiwa kujibu hili ili watu woote wawe huru kukaa na majina yao bila kuadhibiwa kielimu, kijamii, kirafiki, kikazi, kisheria, kihuduma, kibiashara n.k.