Mlezi wa kituo cha kulelea watoto yatima cha Nusuru yatima Bi. Khadija Khalfani akimshukuru Miss Tanzania 2010, Geneiveva Mpangala alipotembelea kituo hicho na kutoa misaada mbalimbali ya vyakula vyenye thamani ya zaidi ya shilingi 700,000 kwa watoto yatima wanaolelewa katika kituo hicho, pamoja na uamazi wake aliouchukua wa kuwasomesha watoto wawili toka katika kituo hicho.
Miss tanzania akiwa katika picha ya pamoja na watoto yatima wa kituo cha kulelea watoto cha Uyacho kilichoko eneo la Hamgembe katika manispaa ya Bukoba.
Miss Tanzania Geneiveva Mpangala akiwa katika picha ya pamoja na watoto yatima wanaolelewa katika kituo cha Nusuru Yatima kilichopo katika manispaa ya Bukoba. Mwenye miwani mweusi Zakia ally ambaye ni msaidizi wa miss Tanzania na mwenye fulana nyeusi ni mkuu wa itifaki wa kamati ya maandalizi ya miss Tanzania Albert Makoye. Picha na Audax Mutiganzi wa Globu ya Jamii, Bukoba
Tumechoka na haya mambo ya maMiss, anzisheni miss and mr Talent, wapelekeni vijana chuo kikuu, wapeni elimu za juu.
ReplyDelete