URBAN PULSE inawaleta Ziara ya Mwenyekiti wa Tanzania Assocciation Uk Dr Lusingi akifanya ziara ya kutembelea Watanzania wafanyao shughuli mbalimbali hapa England. DK.Lusingu alifuatana na Mjumbe wa Nec Bi Asha Baraka ili naye ajionee na kujifunza wayafanyayo Watanzania UK. Kampuni hii ya Computer 4 Africa inamilikiwa na mjasirimali wa Kitanzaniana aitwae Bw Aseri Katanga. Kampuni hii inajishughulisha na ukusanyaji wa kompyuta zilizotumika, kisha wanazikarabati kuziweka kwenye hali ya kuwa mpya, halafu wanazisambaza Afrika nzima. Kompyuta hizi hupelekwa kwenye mashule, taasisi mbalmbali na idara ya serikali. Kwa upande wa Tanzania zaidi ya shule 100 zimesha faidika na mpango huu
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Watanzania Tanz-UK John Lusingu akipata maelekezo kutoka kwa enginer wa kampuni ya computer 4 Africa
Mkurugenzi wa Aset Asha Baraka akikagua baadhi ya computer zinazosafirishwa na kampuni ya Computer 4 africa
mwenyekiti wa Tanz-UK Dk. John Lusingu na Asha Baraka wakiangalia baadhi ya Computers
Mkurugenzi wa Aset Asha Baraka akiteta jambo fulani pamoja na wafanyakazi wa computer 4 Africa na Mwenyekiti wa Tanz-UK
computer zilizofanyiwa urekebishwaji na matengenezo tayari kwa kuingia Africa
Baada ya kumaliza ziara kutoka kushoto Ndg Katanga,
Dk. John Lusingu, Frank Eyembe na Asha Baraka
Wakurengenzi na wafanyakazi wa Computer 4 Africa wakiwa na mwenyekiti wa Tanz-UK Dk. John Lusingu na Mkurugenzi wa Aset Asha Baraka

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 14, 2011

    Je hizo computer zinauzwa au bure? Ukweli kama mdau wa IT computer zenye viwango vya chini ni maudhi matupu, viwango vya RAM, Processor, Graphic cards ni muhimu ili mtumiaji anufaike na application zilizokuwepo sasa.

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 14, 2011

    Napenda kutoa dukuduku langu. Ni vyema kwamba Tanzania tunapata Misaada ya hizi used Komputa. lakini je tunaplan gani in place katika swala zima la environmental impact ya Electronics goods after its life time has ended. Kama mtaalamu wa Electrical na Electronics nadhani watu wanahitaji kuelimishwa katika swala zima la madhara yatakayotukumba in future kuhusu materials zinazotumika kutengenezea Electronics equipment.Mdau Reading UK.

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 15, 2011

    Most people who have taken actions of development have done so sometimes without thinking of the consequensies.In the western world when computers were invented their thoughts were how the computers can revolutionise the way people do things but not the WEEE act from Europe.
    Later when this became a problem someone else started thinking of Recycle & Reuse. That's how people bring development by playing their part rather than thinking one person should think of everything!.
    Since some people know about the environmental impacts of this technology brings, should bring their ideas to the table so that we in Africa can do better than the west in terms of not creating litter.
    Therefore, let us work together for the good of mankind.Yes we can.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...