Mjomba Ankal
Kama unavyo wasaidia wanajamii wengi kutafuta ndugu na jamaa zao. Naomba fadhila hiyo unifanyie nami pia kwani nimepotezana na rafiki yangu kwa jina anaitwa Juma Shabani Kassele. Tulikua wote magamba secondary school.
Wazazi wake ni wenyeji wa Shinyanga sehemu za bariadi nahisi anaweza kua anaishi maeneo hayo. Baba yake mdogo alikua na studio ya picha iitwayo furaha pale Muheza, sijui kama bado inaendelea. Kwa taarifa hizi yeyote yule anaye ujua ukoo wa Kassele anaweza kunisaidia kumpata Juma.
Kama hajabadilisha kazi atakua mahali fulani anafundisha. Kwa anayejua habari zake anaweza kunitumia mawasiliano ya hapa mtandaoni ama katika mobile +4520695430 au kumpatia huyo Mr Juma hizo namba za mobile
Natangulizashukrani.
Mdau Masudi
Dah, jamaa sasa yuko ughaibuni, mbeba boksi mzuri tu. Kanunua banda Karikaoo, anataka kuteremsha ghorofa la floor 15. Kila la heri.
ReplyDelete