Marehemu Mama Aurelia Kinyaiya

Ndugu, Jamaa na Marafiki,

Kwa masikitiko makubwa tunapenda kuwaatarifu ya kuwa mama Aurelia Kinyaiya, amefariki dunia leo Jumamosi [June 11th 2011] Memorial Hospital,Minneapolis Minnesota. Marehemu ni mama mzazi wa Elifaa na David Kinyaiya waishio Minnesota, na Alekunda Mmari aishiye Washington D.C.

Makadirio ya gharama za kusafirisha mwili pamoja na watakaosindikiza kwenda Tanzania kwa ajili ya mazishi ni $25,000.

Kama ilivyo desturi yetu, tunaombwa kuungana na familia ya Kinyaiya katika kukamilisha mipango ya kusafirisha mwili.

Unaweza kutuma mchango wako kwa njia zifuatazo;
1: WellsFargo Bank Wire transfer: Route # 530000509, Ac # 3165545314, Jina: Elifaa Kinyaiya au David Kinyaiya.

2.Western Union & MoneyGram : Zote zitumwe kwa:Neville Lema [612-964-4218].
3.Hundi (cheki) kwa: Elifaa Kinyaia :10716 Scott Avenue N,Brooklyn Park,MN 555443.
Maandalizi ya kusafirisha mwili yanaendelea nyumbani kwa Elifaa & David Kinyaia :10716 Scott Avenue N,Brooklyn Park,MN 555443.

Unaweza kuwasiliana na wafiwa kwa namba zifuatazo:
Elifaa:641-583-1189 ,
David 952-215-1116,
Alekunda 202-375-3847.
Lilian Maina 612-669-2782
Kwa taarifa zaidi, wasiliana na;
Honest Tesha:651-343-3209,
Riwa 952-457-0599,
Mollel 651-334-0163,
Denis Shengena 952-992-9489,
Erick Lemunge 651-398-1861.
Flaviana Tesha 651 329 4521

Bwana Ametoa, Bwana Ametwaa. Jina la Bwana Libarikiwe.
Akhsante,

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 10 mpaka sasa

  1. Mungu awe faraja yenu.
    Roho ya Marehemu Mama Aurelia ipate pumziko la heri.
    Utukufu una Yeye!
    Akifarijini Mwenyezi Mungu!
    Amin.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 12, 2011

    Poleni san a wafiwa.

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 12, 2011

    Naomba nipate maelezo zaidi ya marehemu.Kwo ni wapi na atazikwa wapi?
    kumradi kwa maswali yangu

    ReplyDelete
  4. AnonymousJune 12, 2011

    Asante kwa swali lako. Kwao ni Tanzania, Moshi. Na anatarajiwa kufika Dar-es-salaam 18 June, 2011, then watasafiri tena kwenda kuzika Moshi, Uru,Shimbwe. Sasa hivi msiba upo Mbezi Beach, nyumbani kwa Mzee Kinyaiya.

    ReplyDelete
  5. AnonymousJune 12, 2011

    Mungu awape faraja Elifaa pamoja na familia yote.
    Bwana ametoa na ametwaa, jina la Bwana libarikiwe.

    ReplyDelete
  6. AnonymousJune 12, 2011

    naomba kuuliza huyu mama anaundugu beny kinyaiyas au ni mama yake naomba jibu wapendwa

    ReplyDelete
  7. AnonymousJune 12, 2011

    Ningeshauri tu kuwa mfanye utafiti zaidi wa bei za kusafirisha mwili wa marehemu kwavile inaonyesha kuwa Mnalanguliwa. Watu wameshasafirisha miili toka West Coast for less than 15,000 kwahiyo nadhani wahusika wanatakiwa wafanye utafiti kidogo. 25,000 is just too much. Nadhani hata mdau hapo juu aliyeuliza kuwa kwao marehemu ni wapi alishindwa tu kuwa wazi kuuliza kwanini gharama ni kubwa hivyo. Poleni sana wafiwa.

    ReplyDelete
  8. Asante Kaka Michuzi kwa kutusaidi kusambaza hii habari ya msiba wa mama yetu.
    @Anonymous Sun Jun 12, 07:41:00 PM 2011
    Kwa kwaida yetu tunavyofanya hapa Minnesota huwa tunachangia familia yenye msiba kusaidia kwanza kusafirisha marehemu nyumbani, expenses the funerel home, wanafamilia watakosindikiza mwili, gharama za msiba hapa na nyumbani.
    Asante sana kwa feedback yako na tunashukuru kwa maoni zaidi.

    ReplyDelete
  9. AnonymousJune 13, 2011

    Mungu aipumzishe roho ya Marehemu Mama Aurelia Kinyaiya kwa amani,Alikuwa ni mama mkarimu na mchangamfu sana,Mungu awape nguvu watoto wake wote Tauka,Alekunda,Siana,Elifaa na David pamoja na Mume wake Mzee Ferdinand Kinyaiya.

    ReplyDelete
  10. AnonymousJune 15, 2011

    @Anonymous Sun Jun 12, 05:51:00 PM 2011, sio Mama yake Ben Kinyaiya, ila wana undugu.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...