Shujaa wa Vita ya Pili ya Dunia Mzee Ernest Paulo Waya akiongea na Globu Dada ya Jamii, Mbeya Yetu, amesema serikali imewatelekeza na kutowajali kwa chochote na kuwazulumu mafao yao mashujaa hao wa zamani ila huwaona wa maana sana siku ya mashujaa tu ambapo amesema huwaita ili washiriki pamoja siku hiyo. Amedai kwamba  zoezi hilo likiisha huwa wanatelekezwa mpaka mwaka mwingine tena. Mzee Waya amesema ndiyo maana mwaka huu wenzake wengi hawajaja kwani wapo kujitafutia riziki maana kula yao ni ya shida sana
Mzee Ernest Waya akiweka upinde na mshale kuwakumbuka wenzake aliokuanao vitani enzi hizo
Mzee Ernest Waya akitoa heshima mara baada ya kuweka upinde na mshale
Toka kushoto ni Mkuu wa Mkoa Mbeya John Mwakipesile wapili ni Mstahiki meya wajiji la Mbeya Mh Atanas Kapunga watatu Mzee Ernest Waya wanne ni mwakilishi wa machifu wa Mbeya
Shughuli imekwisha Mzee Waya huyooo ndiyo wamekwisha msahau hawana mpango nae tena. Hapa anaelekea ofisi ya mkuu wa Mkoa Mbeya apate msaada wa usafiri kumrudisha kwake Mbalizi

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 18 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 26, 2011

    HUYU MZEE ANATIA HURUMA SANA. KAMA WAHUSIKA WANA MASIKIO BASI WAMESIKIA. YAANI HATA USAFIRI WA KUMRUDISHA KWAKE HAWAKUMPATIA?

    BILA SHAKA NAYE MWAKANI ATAINGIA MITINI NA KUSUSIA SHEREHE HIZI.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 26, 2011

    Lakini walipigania vita muingereza ili azidi kututawala sasa wapeleke malalamiko yao ubalozi wa uingereza. Pia UK Tanzania wafikishe malalamiko kwa mama maana hao ni wenzao isipokuwa tu wamemtumikia wakati tafauti!!

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 26, 2011

    Sidhani kwamba ni haki kuwalaumu wao kwani kwa kipindi kile ndiyo mfumo uliokuwepo.

    Pia mdau ukumbuke vile vita vya pili walivyopigana nchi tofauti ndiyo vilivyowaamsha na kuwaelewesha kwamba kumbe hata Wazungu nao hupigika. Na ndipo harakati za kugombania uhuru zilipoanza.

    Niliwahi kusikia kwamba walikuwa wameletewa pensheni zao pamoja na fedha na maangalizi ila kuna kipindi serikali iliwahi kuwadhulumu. Mwenye ukweli atujuze. Hii ni sawasawa na ile ya Afrika Mashariki kwani fedha zilizoletwa zilitumika kwa mambo mengine na mpaka leo wanataseka na kufa pole pole.

    ReplyDelete
  4. AnonymousJuly 26, 2011

    kwanza hao waliomuita ni wauwaji sana malipo hapahapa mimi angekuwa mzee wangu nisingemuruhusu anaambulia kula chakula cha siku moja na mkuu wa mkoa alafu anarudi kulala chini anafuatwa na gari kurudi kwa miguu huo ushahidi tosha hapo anatembea anaelekea kwake hiyo njia inaelekea kwa mama john mbeya ndo anaishi kule karibu na mzee mmoja nae alikuwa mkubwa siku hizi analima maparachichi

    ReplyDelete
  5. AnonymousJuly 26, 2011

    Nafikiri huyu ndiye Sikamona niliyemsoma katika kitabu cha ZAWADI YA USHINDI cha Amandina Lihamba

    ReplyDelete
  6. AnonymousJuly 26, 2011

    Kuna pesa zilikuwa zinatolewa na serikali ya Uingereza lakini wajanja wa serikalini wakawa wanazila.Nchi yetu haina huruma kamwe

    ReplyDelete
  7. AnonymousJuly 26, 2011

    Serikali ingekuwa imemtelekeza angekuwa katakata hivyo? na suti ya nguvu hivyo?

    ReplyDelete
  8. Anon, Zawadi ya Ushindi kiliandikwa na Amandina Lihamba au Ben Mtobwa?

    ReplyDelete
  9. Miaka ya 80, kuna chama fulani cha Royal Commonwealth, iliyowasafirisha waliopigana WWI kwenda Uingereza kwenye sherehe. Pia pale Faya Dar kulikuwa na Club ya hao WWI na WWII veterans. Hivi bado ipo? Najua kuwa wote waliopigana WWI wamefariki, je, hao wa WWII waliobaki wako wapi? Tunapaswa kuona hao waliobaki mali. Sasa huyo Mzee anatembea na gongo anakwenda kuomba lifti, ni aibu tupu!

    Na ni kweli serikali ya Uingereza walileta hela ya kuwasaidia hao Veterans lakini pesa zilipita serikalini kwanza na hao wazee walipata kiduchuu!

    ReplyDelete
  10. AnonymousJuly 26, 2011

    Why is the Head Chief wearing a Joker's Hat? Looks like a Halloween Costume!

    ReplyDelete
  11. AnonymousJuly 26, 2011

    Ha ha ha wacha mbavu sina, mdau wa halloween umegusa haswa, huyo chifu ni mjukuu wake alimletea hiyo kofia wakati wa likizo na chifu akai-mind sasa kaivaa wakati wa hafya ya kitaifa basi we sisi mbavu hatuna, lakini si haba watu wengi walioudhuria na wanaosoma hii blogu hawakugundua kuwa ile kofia ilikuwa ya Joker!!!!
    alex bura, dar

    ReplyDelete
  12. AnonymousJuly 26, 2011

    hiyo ndio bongo ya dasalame ya wadanganyika bana nyingine ni feki kula chako mapema ukimaliza muda wako saga inakusubiri

    ReplyDelete
  13. AnonymousJuly 26, 2011

    Wazee wote nchini wamechoka wa wliopigania WWII, uhuru na wazee kwa ujumla. Malipo yao walilipwa na serikali ya Uingereza ni nani aliyenaudhibitisho kuwa serikali iliwadhulumu? Wazee kama hao wa kenya wanaenda Uingereza kudai kama wanaona wamedhulumiwa. Kwa wasio na uwezo wa kusafiri basi wanaenda kwenye barozi zinazohusika. Ila serikali inapo muita kujumuika kwenye sikukuu yao lazima watakuwa wamepewa suti nyeusi, nauli na malazi na mapochopocho mengine. Mzee huyo baada ya kumaliza shughuli na kwa kuwa kisha pata chake inabidi aanze safari kurudi. sio tena kudai gari kama maelewano ni yalikuwa hivyo. Hivyo wadau tusikuze mambo PESA TAMU

    ReplyDelete
  14. AnonymousJuly 26, 2011

    juzi walitakiwa waliopigana vita vya dunia wakale pensheni yao kama ana akili huyu akusanye wenzake na ushahidi aende ubalozi wa uk tu huwenda pia akahitimu maisha yake huku huku UK.
    uMRI WAO NA VIONGOZI SAWA SAWA LAKINI UKIMUANGALIA UTAFIKRI ANA MIAKA 100

    ReplyDelete
  15. AnonymousJuly 26, 2011

    Mbona hujasema UMRI WA HUYU MZEE? NI MHIMU SANA TENA SANA.

    ReplyDelete
  16. Babu yangu mpaka anakufa alikuwa akiniadithia jinsi walivyozulumiwa pesa zao zilitoka kama sikosei uingereza lakini kuna siku sisi wajukuu zao tuta dig in na kutafuta nini hasa kilitokea na kama ni kweli ni akina nani hasa wanausika na ulaji huu ili sheria ichukue mkondo wake pole sana babu nasikia uchungu kwani wewe ni sawa na babu yangu kabisa pole sana.

    ReplyDelete
  17. AnonymousJuly 27, 2011

    daa iyo ndio serekari ya tz wajanja wengi sana kila mtu anakula upande wake

    ReplyDelete
  18. AnonymousJuly 27, 2011

    wengine mpaka leo wanandika majina na wengine wameshaandika zaidi ya mara kumi hasa kipindi cha uchaguzi

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...