Na:- Azizi Simai  Maelezo Pemba.
 
Balozi Mdogo wa China Zanzibar,  CHEIN CHIN MAN amesifu uhusiano uliopo kati ya China na Zanzibar kutokana na mashirikiano makubwa waliokuwa nayo tangu Mapindzi ya mwaka 1964.

Amesema China itaendelea kusaidia Zanzibar katika nyanja mbali mbali za Maendeleo katika juhudi za kukuza Uchumi wake pamoja na Wananchi .
 
Balozi CHEIN ameyasema hayo katika Ghafla ya kukabidhi Hundi ya Shillingi Millioni  Ishirini kwa Skuli Tatu ziliopo katika Jimbo la Mkanyageni Wilaya Mkoani Pemba kwaajili ya Vifaa vya Sayansi, Msaada ambao umetolewa na Kampuni ya Mawasiliano ya Kichina ya HUAWIE.
 
Kampuni hiyo ya HUAWIE  imesaidia Fedha hizo kwa ajili ya Skuli ya CHOKOCHO,KISIWA PANZA NA MKANYAGENI baada ya kuombwa na Waziri wa Mawasiliano ya Sayansi na Teknolojia wa Tanzania.
 
Nae Waziri wa Sayansi na Teknolojia wa Serikali ya Muungano Tanzania Professa Makame Mbarawa Mnyaa amewataka Vijana Maskulini kuvitumia Vifaa vya Sayansi kwa kuliwezesha Taifa kuwa na Wataalamu wa fani Mbali mbali.
 
Waziri huyo amesema kuwa ili Taifa liwe na Wataalamu Wazuri ni muhimu Vijana Maskulini kuzitumia vyema Maabara na Vifaa vilivo kwenye Skuli zao na kuvienzi Vifaa hivyo iliviweze kuwasaidia  na wengine.
 
Aidha Professa Mnyaa amesema Taifa lolote Duniani ili liendelee linahitaji Vijana waliofanikiwa kwa kiasi kikubwa katika Masomo ya Sayansi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. Tsh. 20 million is less than $20,000. Is this from his own pocket or from the government of China?? In exchange for what??
    Really do we need to publish such meager amount when what they reap from us in comparison to his/their $20,000 is just a drop in the ocean!
    We need to be serious!
    Homer

    ReplyDelete
  2. i agree wit you,the first coment,even they representative ,he/she might givin them concern those school $20,00o , i think this kind of joke from chinies for given them $20,000 . they have to be seriously,it's shame to publish .

    ReplyDelete
  3. Little, little lastly make jug full.

    ReplyDelete
  4. "little, little lastly make jug full" - Kide,

    Well that's why people steal from us, treat us like bunch of incompetent people.Even our own politicians steal from us in broad daylight cause they know we will always find an excuse for their action

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...