Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mh Samwel Sitta (shoto),  Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Mh William Lukuvi (kulia) na kaimu Katibu wa Bunge wakipanga mikakati ya kufanikisha shughuli hii ya msiba katika hospitali ya Mkoa wa Dodoma kufuatia ajali ambayo alipata 
Mbunge mteule kutoka Baraza la Wawakilishi Zanzibar,Mussa Khamis Silima, alipata ajali juzi katika eneo la Nzuguni, Dodoma, ambapo mkewe, Mwanaheri fahari,  alifariki dunia na yeye na dereva wake kujeruhiwa vibaya na kukimbizwa hospital ya Muhimbili kwa matibabu zaidi
 Mwili wa mke wa Mbunge Mussa Khamis Silima, Hayati Mwanaheri, ukiombewa dua na Wabunge n waombolezaji wengine baada ya kuwasili katika Msikiti Mkuu wa Ijumaa mjini Dodoma leo kuswaliwa kabla ya kupelekwa Zanzibar kwa mazishi. Marehemu alifariki Jumapili jioni kwa ajali ya gari  katika eneo la Nzuguni, nje kidogo ya mji wa Dodoma
 Mwili wa Marehemu ukiingizwa msikitini kuswaliwa kabla ya safari
 Gari la mafuta lililohusika katika ajali hiyo ambapo mfanyakazi wake anaonesha mahali ambapo gari dogo lililokuwa na marehemu na mumewe kugonga wakati likitaka kupita
 Mmoja wa mashuhuda wa ajali hiyo akimweleza mbunge wa Mafia, Mh Shah, kilichotokea
 Mbunge wa Mafia Mh. Shah akiliangalia gari dogo la Mh. Silima lilivyoharibika baada ya ajali hiyo
Baadhi ya wabunge wakiwa chumba cha maiti cha hospitali ya Dodoma kusubiri kuchukua mwili wa marehemu
Dereva Chezani Sebunga aliyekuwa akiendesha gari la Mbunge, Mussa Khamis Silima na kupata ajali eneo la Nzuguni, Dodoma , akiwa katika machela akiingizwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili leo asubuhi, akitokea mkoani Dodoma. Mke wa Mbunge Silima, Mwanaheri Fahari alifariki dunia katika ajali hiyo. Mbunge mteule kutoka Baraza la Wawakilishi Zanzibar,Mussa Khamis Silima, ambaye alipata ajali juzi katika eneo la Nzuguni, Dodoma, akiwa katika machela baada ya kushushwa kwenye gari jana katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, akitokea Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es Salaam, alikoletwa na ndege kutoka Dodoma. Mke wake, Mwanaheri Fahari alifariki na dereva wao Chezani Sebunga alijeruhiwa kwenye ajali hiyo. Kwa picha zaidi BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 7 mpaka sasa

  1. Poleni kwa Msiba. Barabara zinazojengwa hazina std. Ni nyembamba mno

    ReplyDelete
  2. Wembamba wa barabara si sababu ya msingi ila ni maamuzi sahihi ya madereva

    ReplyDelete
  3. nimesikia na mh mbunge amefariki mchana huu....pole kwa wanafamilia

    ReplyDelete
  4. Kuna barabara nyembamba kama UK? Lakini sheria zake zilivyo kali mwenyewe utaendesha kwa adabu. Sheria za kwetu bado sana na watu hawaogopi hiyo adhabu ndogo. Nazungumzia barabara ambazo sio highway. Na vile vile wasingesafiri usiku jamani its too risk kwa sababu ni muda ambao magari makubwa yanaruhusiwa kusafiri. All in all innallillahi wainaillaihi rajiun

    ReplyDelete
  5. SHEIKH MICHUZI,
    HIVI MTU ANAPOKUKABIDHI KITU CHAKE UMUUZIE NADHANI UTAKIUZA KWA BEI ITAKAYOKUWA SAWA AU JUU YA BEI ALIYONUNULIA AU GHARAMA YA KUTENGENZEA. SASA IWEJE SERIKALI IWAKAMATE WATENDAJI WA BP ILIHALI WATENDAJI HAO WALIOMBA RUHUSA KWA SERIKALI IWARUHUSU WATENDAJI WAUZE KWA BEI YA HASARA KAMA EWURA ALIVYOKURUPUKA KUITANGAZA HADI LEO SERIKALI HAIJATOA IDHINI HIYO. NADHANI HAPA PANABIDI MJADALA ILI WATANZANIA WAELEWE UKWELI. JEE SERIKALI ITAWEZA KUJISHTAKI YENYEWE?

    ReplyDelete
  6. kila kitu kinataka sibabu huwo ndio mwisho wa binadamu RIP.

    ReplyDelete
  7. huwo ndio mwisho wa binadamu, kila kifo kinataka sibabu RIP

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...