Wakazi mamia waliohudhuria onyesho la Parapanda katika tamasha kubwa la Utamaduni la Sweden jijini Gothenburg, ambapo shangwe na chereko zilimeza uwanja huo wakati wasanii hawa alipokuwa wakiunga kazi moja baada ya nyingine.

Onesho hilo limefanyika leo jioni saa 11.30 hadi saa 12.00 juu ya alama mbele ya umati ambao uliomba kurudiwa kwa onyesho lakini kwa kweli isingewezekana kwani  kuna vikundi zaidi ya 10 vinasubiri! Hili lilikuwa ni onyesho la kutambulisha onyesho kubwa la NATIGONE litakalofunguliwa rasmi hapa tarehe 8 Oktoba

Shabo Makota akicharaza gitaa
Eva Nyambe, Frank Samatwa na Amani Lukuli wakilishambulia jukwaa

Daudi Joseph akicharaza  Jembe  ngoma yenye asili ya Afrika Magharibi.

Eva Nyambe na wenzie wakishambulia jukwaa


Eva Nyambe akipagawisha watasha
Fujo Makaranga mtalamu wa kupiga ngoma ambaye naye yuko Sweden  kikazi akimpongeza Daud Joseph wa Parapanda  baada ya kazi nzuri jukwaani. Nyuma yake ni Binti wa Kiswidi ;Cameila ambaye "amewatoa" vijana wengi wa Tanzania katika fani ya ngoma na hasa za ubunifu. Anayeangalia ni Mkurugeni wa Gothernburg City Theatre Ronnie hallgren

Ronnie akimpongeza Kiongozi wa Parapanda na Mwongozaji Mwenza katika tamthiliya ya Antigone bwana Mgunga Mwa Mnyenyelwa.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Hongera sana PARAPANDA ART THEATRE hakika mmeiwakilisha Nchi yetu vizuri. Sisi wazawa hatutambui mchango wenu lakini wageni wameona pia wametambua umuhimu wenu kazeni buti ipo siku isiyokuwa na jina nanyi mtafaidi matunda ya kazi na uvumilivu wenu. Achaneni kabisa na viongozi wetu wala rushwa wasiotambua mchango wenu katika taifa hii.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...