Na Mwandishi wa Jeshi la Polisi, Zanzibar

Polisi Visiwani Zanzibar wamekamata Shehena kubwa ya Pembe za ndovu katika Bandari ya Malindi Visiwani hapa.

Hii ni  Shehena kubwa ya kwanza kukamatwa katika Visiwa vya Unguja na Pemba ambapo Polisi walifanikiwa kuigundua baada ya taarifa za Kiintelijensia zilizofanyiwa kazi kitaalam.

Shehena hiyo ya Vipusa ilikuwa imepakiwa  katika makontena mawili huku kukiwa na shehena ya samaki aina ya dagaa wa maji baridi.

Taarifa ambazo bado hazijathibitishwa na Mamlaka husika, zinadai kuwa Shehena hiyo ya Pembe za Ndovu ilikuwa ikipelekwa nchini Malaysia.Hadi saa 1:00 usiku Polisi walikuwa wakiendelea na kazi ya upakuaji na upekuzi zaidi katika eneo la Bandari ambapo kwa mujibu wa Mkuu wa Polisi Bandarini, Martin Lissu watu wawili wanashikiliwa na Polisi kwa mahojiano zaidi.

Watu waliokamatwa ni pamoja na Wakala wa mizigo ambaye Polisi wamesema ni mapema mno kumtaja kwa sababu za kiupelelezi

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...