Mwenyekiti wa timu ya simba aliyevaa tisheti nyekundu Godrefy Nyange Kaburu akiwa amewatembelea mashabiki wa timu ya Yanga waliouthuria Tamasha la Simba uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha na  wakibadilishana mawazo
 Makamu Mwenyekiti wa Simba Godfrey Nyange Kaburu akiongea na wana Yanga
 Mshabiki wa timu ya yanga aliyetambulika kwa jina moja la Rama Yanga akiwa  amekwidwa na washabiki wa timu ya Simba kwa kuingia kwenye tamasha la simba na kukaa upande wa wana Msimbazi akiwa na jezi ya Yanga  
 Mashabiki wa Simba toka Dar es salaam  wakiwa wanashangilia mara baada ya timu yao kuingia uwanjani
 mashabiki wakishangilia kwa nguvu
 Mkurugenzi  wa Tanapa  Allan Kijazi akiwa na Makamu Mwenyekiti wa timu ya simba  Godfrey Nyange Kaburu wakitambulisha jezi mpya ambayo timu hiyo itaitumia katika msimu wa ligi ujao
Mgeni rasmi wa tamasha hilo ambaye ni mkurugenzi wa Tanapa  Bw. Allan Kijazi akiwa anasalimiana na wachezaji wa timu ya Victors  wa Uganda wakati akikagua timu. Katika mchezo huo Victors iliifunga Simba bao 1-0 kwa njia ya penati. 
Picha zote na Woinde Shizza wa Globu ya Jamii

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. kwa kweli unajua kila siku huwa tunasema Simba akili zao kama sisimizi watu wanabisha. Huyu wanayemsukuma na kumpiga walitakiwa wampe hongera na wamsifu kwa kuonyesha kuwa ni mwanamichezo. kalipa kiingilio ili kuwaunga mkono watani zake na kujumuika pamoja kama mwanamichezo. lakini la kushangaza wanampa kichapo. kama sio ujinga na ushamba ni nini?! kwani siku ile walisema/walitoa tamko kuwa ni kwa ajili ya Wanasimba tu?! maana kwa mujibu wa matangazo waliyoyatoa ni kwamba watu wote tulikuwa tumealikwa na tena kwa kiingilio.
    SIMBA ACHENI USHAMBA!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...