Mitambo iliyowasili leo na kazi ya kuifunga itatarajiwa kuanza hivi karibuni. Akielezea zaidi kuhusu ujio wa mitambo hiyo ya Aggreco, Badra alisema kuwa hii ilikuwa ahadi ya Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja, alipokuwa akiwasilisha bajei ya wizara yake Bungeni hivi karibuni. Mipango mingine ya kumaliza mgao wa umeme ifikapo Disemba mwaka huu ni pamoja na kutumia mitambo ya Symbion yenye uwezo wa kuzalisha Megawati 112, na mitambo ya Jacobsen inayoendelea kufungwa hatua inayoipa Tanesco uhakika wa kumaliza kero ya mgao wa umeme mwezi Disemba mwaka huu
Home
Unlabelled
tanesco yakamia kumaliza mgao wa umeme nchini ifikapo desemba mwaka huu
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Hapa ndipo Tanesco wanaponifurahishaga...Hivi shida ya nchi ni Mitambo ya kufua umemeeee? au ni vyanzo vya nishati..mfano maji, gesi, mafuta na nishati nyinginezo???? Hebu Tanesco mtupe njia mbadala(Alternatives)zote, upatikanaji wa nishati pia ni muhimu, sio inafikia mahali mnasema eti mnazima hiyo mitambo halafu fedha ya kuazima mitambo mnaendelea kuwalipa wenye mitambo. Acheni tu kutoa majibu yasio na solution huko mbeleni. Rais alihojiwa na BBC kuhusu upatikanaji wa Umeme, akajibu "Tanzania haina uwezo wa kufanya Mvua inyeshe"...hivi ni issue ya mvua au ni issue ya mipango mibovu na isiyo endelevu???....Hebu acheni kutufumba na viji-mitambo vyenu vya kukodi hapa! Mnaboa sana!
ReplyDeleteYale yale mliyokuwa mnasema kipindi kile gesi ya Songo songo ilipoanza kuzalishwa, na bado mnasema hivyo hivyo.. Tunajua pasipokuwa na mgao vibosile wengi watakufa njaa.
ReplyDeleteWakwanza umenena CHANGA LA MACHO
ReplyDeletejamani mimi ndio sielewi au
ReplyDeletetatizo la umeme lilikua kwasababu ya vyanzo vya nishati kama maji kupungua sasa kama maji yamepungua na Tanzania hatuwezi tengeneza mvua kama Raisi alivyosema iyo mitambo inakodishwa ili ifue umeme kutoka vyanzo gani au mimi ndio sielewi jamani?
au ndio yale yale ya viini macho kukodisha mitambo mradi wa watu flani wanapata kula kwao kama ilivyokua kwamitambo mingine
mmhhh Tanzania kazi ipo
Nauliza hivi ,hili tatizo la umeme hapo disember likimalizika litadumu kwa muda gani ? Au baada ya miezi 6 mgao mpya tena wa umeme ? Tunafahamu kuwa kila mwaka au baadaya miaka 2 matatizo haya huwa yanajirudia kila mara.
ReplyDeleteMichuzi tunakuomba utupatie habari kamili juu ya tatizo la umeme kumalizwa ni la muda gani ? Tumechoshwa kuburuzwa na hawa Tanesco. Kamavipi tujiandae na mitambo yetu wenyewe bila ya kutegemea mitambo ya tanesco ambao umekuwa kero toka kupata uhuru.
Kwa nini mitambo ikodishwe? Tanesco haina uwezo wa kununua mitambo yake yenyewe?
ReplyDeleteHii inaitwa majoring on minors au danganya toto. Nadhani watanzania hatuhitaji tena hotuba au press conference, Tanesco na au 'mkubwa' yeyote wasizungumzie ufumbuzi wa umeme utatokea lini... tunataka kuuona ufumbuzi bila maneno mengi tumechoka na uongo wa hawa jamaa wakubwa kwa wadogo. toeni tu ufumbuzi bila maneno.
ReplyDelete